To Chat with me click here

Tuesday, September 4, 2012

MNYIKA ‘AMKABA’ WAZIRI ATOE AHADI

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, amemtaka Waziri wa  Fedha na Uchumi Dk, William Mgimwa kueleza ni lini atatoa fedha za kugharimia miradi ya ujenzi wa madaraja makubwa, katika Kata ya Msigani, Manispaa ya Kinondoni.

Mnyika alitoa kauli hiyo mwisho mwa wiki iliyopita wakati akiwa katika ziara iliyoambatana na ufunguzi wa matawi ya Chadema ndani ya chama hicho.

Akizungumza na wananchi wa Mbezi Malamba Mawili, mbunge huyo alisema baada  Benki Kuu ya Tanzania  kutangaza kuvuka lengo katika ukusanyaji  kodi, ni vyema Waziri wa fedha akaeleza lini atatoa fedha za ujenzi wa madaraja hayo.

Alisema yeye akiwa mbunge anayewawakilisha wananchi  wa Msigani, aliamua kufuatilia Hazina, ili kupata  Sh500 milioni kwa ajli ya ujenzi wa  wa madaraja mawili katika kata hiyo.

Alisema hata hivyo, hakufanikiwa kupata fedha hizo.

“Wananchi wana matatizo ya vivuko yakiwamo madaraja na kwa kutambua umuhimu wa vitu hivyo waliniagiza kufuatilia na nikafanya hivyo, lakini bila mafanikio,” alisema Mnyika.
Alifafanua kuwa alimuomba Waziri wa Fedha na Uchumi, kusaidia upatikanaji wa fedha hizo  ili kufanikisha  ujenzi wa madaraja, lakini hakujawa na mafanikio.

Alisema ni jambo la kushangaza kuona wananchi wanapata taabu nyakati za mvua wakati kuna fedha zinazotokana na kodi.

No comments:

Post a Comment