To Chat with me click here

Tuesday, September 11, 2012

RAIS KIKWETE KATIKA UFUNGUZI WA CHUO CHA TAIFA CHA ULINZI

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi Chuo cha UIinzi (National Defence College) Jana Septemba 10, 2012 Kunduchi jijini Dar es salaam. Kulia kwake ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange na kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo hicho, Meja Jenerali Charles Makalala na kushoto kabisa ni aBalozi wa China nchini Tanzania Mhe. Lu Younqing.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Mkuu wa Chuo cha UIinzi (National Defence College) Meja Jenerali Charles Makalala Jana Septemba 10, 2012 baada ya kumkabidhi mfano wa funguo kama ishara ya kufungua rasmi chuo hicho kilichopo Kunduchi jijini Dar-es-Salaam. Kulia ni Mkuu wa Majeshi ya ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkuu wa Chuo cha Ulinzi (National Defence College) Meja Jenerali Charles Makalala baada ya kufungua rasmi chuo hicho kilichopo Kunduchi jijini Dar-es-Salaam, nyuma yao ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa Mhe. Shamsi Vuai Nahodha anayefuatana na mkuu wa majeshi ya Ulinzi Jenerali Davis Mwamunyange
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisoma hotuba yake kufungua rasmi Chuo cha ulinzi (National Defence College) kilichopo Kunduchi jijini Dar-es-Salaam, pamoja na kuzindua kozi ya kwanza ya mwaka mmoja. 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipozi kwa picha ya pamoja na wanachuo wa kozi ya kwanza ya mwaka mmoja katika chuo cha ulinzi alichofungua rasmi hapo jana septemba 10, 2012 Kunduchi jijini Dar-es-Salaam. 
Picha kwa hisani ya: IKULU

No comments:

Post a Comment