To Chat with me click here

Monday, September 10, 2012

CHADEMA YAENDELEZA WIMBI LA KUIBOMOA CCM – UKONGA


Mhe. Kattikiro akiwa jukwaani akinadi sera za chama chake

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Jimbo la Ukonga jana kiliendeleza kile kilichokiita Mwendelezo wa uvunja na kuibomoa ng’ome ya CCM jimboni humo, katika harakati zake za kukiimarisha chama zaidi kwa operations zake za M4C.

Katika mkutano huo wa hadhara uliofanyika viwanja vya mzambarauni, mgeni rasmi aitegemewa kuwa Mhe. Joshua Nassari (MB), lakini hakuweza kutokea kutokana na kuwa na kikao cha Kamati Kuu ya Chama hapo jana. Hivyo basi wapambanaji wengine walishika nafasi hiyo ya kuendesha vuguvugu hilo la mabadiliko ambapo Diwani wa Viti maalumu, Mhe. Grace Shellukindo, Mhe. Maxmillian Kattikiro, Mwk. Wa Chadema Jimbo ndg. Michael Aweda, Katibu wa Jimbo ndg. Mwaipopo, Mwk. Wa Kamati ya Wahanga wa Mabomu G/mboto ndg. Obadia, aliyekuwa mgombea ubunge Jimbo la mvomelo ndg. Matokeo, Advocate Nixon, Mwk. Wa Bavicha Jimbo, ndg. Fredrick Kabati na wengine wengi walikuwepo ili kuweza kuisambaratisha vilivyo ngome hiyo ya CCM ambapo walifaulu kwa kiasi kikubwa sana. 

Akiongea katika mkutano huo Mhe. Kattikiro aliwataka CCM kuacha siasa chafu za kuchafuana zinazoendelezwa hivi sasa na watawala wetu na kusisitiza ni vyema watawala wakajikita zaidi katika kutafuta ufumbuzi juu ya kuwakwamua Watanzania toka katika wimbi kubwa la umasikini walilonalo. 

Aidha aliongeza kuwa, Tanzania ni nchi tajiri kuliko zote duniani, lakini utajiri wake umekuwa ukiwanufaisha watu wachache wenye madaraka na wageni ambao huingizwa nchini kwa kofia ya uwekezaji. 

Akitoa mifano kadhaa, alinukuu kauli ya Mheshimiwa Rais wa Rwanda, Paul Kagame kuwa, “kama nchi yangu ingepewa bandari hii ya Dar-es-Salaam pekee, basi ningeweza kuifanya Rwanda moja ya mataifa tajiri mno duniani” hivyo alihoji je Tanzania tunabandari ngapi? Mtwara, Tanga, Zanzibar na Dar-es-Salaam, Je viongozi wetu hawana mawazo ya nini kifanyike kwa kutumia raslimali hiyo ya bandari kuweza kuinua uchumi wetu? Au vichwa vyao (Viongozi) vinautofauti gani na kichwa cha Kagame kuwa yeye awe na uwezo huo lakini watanzania tusiwe nao? Alihoji. 

Alisema, “Kauli ya Kagame, ilikuwa ikituambia watanzania kuwa, viongozi wenu mliowachagua (CCM) hawana nia ya dhati ya kuwakwamua toka kwenye umaskini uliowagubika watanzania, wako kwa ajili ya manufaa yao binafsi na ndiyo maana wameshindwa kutumia fursa mbalimbali za raslimali kemkem ambazo Tanzania imetunukiwa na Mwenyezi Mungu bure”.

Katika Mkutano huo wa hadara CHADEMA ilikuwa inawakaribisha wanachama wapatao 46 toka CCM na vyama vingine vya upinzani ambapo walisarimisha kadi zao kwa Mwenyekiti wa Jimbo Mhe. Aweda naye kuwakabidhi kadi ya chama hicho. 

Awada aliwapongeza sana makambanda hao wapya, ambao wameamua kishujaa kikihama chama tawala (Kuvua Gamba) na kuhamia chadema (Kuvaa Gwanda). 

Akizungumza kwa niaba ya wanaCCM ambao walijisalimisha kikamilifu kwa makamanda hao wa CHADEMA ambao walikuwa wakiendesha oparesheni hiyo, aliyekuwa Mwenyekiti wa Vijana wa CCM, alisema, 

“Tunawashukuru sana wanaCHADEMA kwa kutukaribisha CHADEMA, kwani CCM hakuna jipya ambalo sisi ambao tulikuwa wanachama wake tunaweza kulisema na kulisimamia. Kikubwa ambacho tumekiona huko (CCM) ni ufisadi na ubadhilifu wa mali za umma, wamekuwa wakijinufaisha wenyewe huku sisi wananchi tukibaki maskini siku hadi siku”. 

Hivyo aliwataka wanaCCM wengine ambao bado wanasitasita kukiunga mkono CHADEMA, wajitokeze na wasihofie mafisadi, kwani hawana nafasi tena katika nchi hii, kwani kwa miaka 50 ya utawala wao hakuna uwiano na maendeleo yaliyo fanyika kulinganisha na raslimali tulizonazo.
 
Habari katika Picha zaidi tafadhali bofya hapa.....
 Kamanda Kattikiro akitoa maelekezo fulani katika mkutano huo
 Viongozi wa Jimbo wakibadilishana mawazo



 Mshereheshi wa mkutano wa hadhara wa CHADEMA ndg. Ramadhani Mgaya akiwa kazini
 Poweeeeer .... kama ionekanavyo makambanda wakiitikia salamu
 Baadhi ya Viongozi wa Chadema ngazi ya Jimbo wakiwa wanfuatilia kwa ukaribu toka kwa msemaji.
 Sehemu ya Wananchi na wanachama wa CHADEMA waliojitokea kusikiza makamuzi hapo jana.
 Mhe. Grace Shellukindo, Diwani wa Viti Maalum, Halmashauri ya Manispaa ya Ilala akifunguka.

 Katibu Mkuu wa Jimbo la Ukonga Mhe. Mwaipopo akimwaga sera za kuwaponda mafisadi.
 Mwenyekiti wa jimbo, Mhe. Michael Aweda, naye hakubaki nyuma kuungana na wenzake kuisambaratisha CCM
  Waliokuwa wanachama wa CCM, wakipokelewa na Mwenyekiti wa Jimbo, pia wakikabidhi vilivyokuwa vielelezo vyao vya U-CCM kwa chama hicho huku wakishuhudiwa na watu.
 Tukibadilishana mawazo wakati wa mkutano huo na Advocate Nixon, juu ya mambo kadha wa kadha.

No comments:

Post a Comment