To Chat with me click here

Saturday, September 8, 2012

M4C YA CHADEMA JIMBO LA UKONGA


Baada ya RPC na wapelelezi Mkoa wa Dar-es-Salaam kuhairisha mkutano wa M4C Chadema Ukonga, ambao ulikuwa ufanyike siku ya juamosi Tarehe 08/09/2012, kwa madai na visingizio vya Sensa, sasa mkutano huo umepangwa kufanyika siku ya Jumapili ya tarehe 09/09/2012, maeneo ya Mzambarauni Ukonga. 

Hivyo wadau wote na wapenda maendeleo mnaalikwa kuhudhuria na kushiriki kikamilifu kwenye mkutano huo utakao anza majira ya saa nane mchana na kumalizika saa kumi na mbili jioni. 

Mhe. Joshua Nassari Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki ndiye atakaye kuwa mgeni rasmi, akisindikizwa na wanasiasa vijana chipukizi katika jukwaa hilo kama Mhe. Maxmillian Kattikiro, Mhe. Kabati, Mhe. Mwaipopo na wengine wengi. 

Njoo tushiriki pamoja kujadili maendeleo ya Jimbo na Nchi yetu, kwa manufaa yetu, watoto wetu na vizazi vijacho. 

CHADEMA ngazi ya Jimbo inapenda kutanguliza shukurani zake za dhati kwenu nyote na...

KARIBUNI SANA...........PEOPLESSSSSSSSSSSS.............

No comments:

Post a Comment