To Chat with me click here

Friday, September 14, 2012

HAPPY BIRTHDAY MHE. FREEMAN MBOWE

Mhe. Freeman A. Mbowe
Leo ni siku ambayo Mhe. Freeman Aikaeli Mbowe, ametimiza miaka 51 tangu kuzaliwa kwakwe, vilevile anatimiza miaka 21 ya kuongoza Upinzani katika mapambano ya ukombozi wa Taifa letu toka katika makucha ya mafisadi wachache ambao wamekuwa wakilifilisi Taifa kwa kijilimbikizia mali na kuwaacha watanzania wakiwa maskini siku hadi siku. 

Katika harakati zake hizi za kisiasa katika kutetea wanyonge na kulihakikishia Taifa hili ukombozi kamali na wa kweli, Mhe. Mbowe amekuwa akikumbana na changamoto mbalimbali kama vile, kushtakiwa, kusingiziwa mambo mbalimbali kwa chama chake n.k 

Lakini katika haya yote ameendelea kuonesha msimamo dhabiti wa kutetea na kusimamia kile ambacho yeye binafsi na Chama chake kwa pamoja wamekuwa wakiamini. Hii imeonesha dhamira ya dhati ya Mhe. Mbowe katika kuleta mageuzi ya kisiasa nchini ili kutoa fursa sawa ya kimaendeleo kwa kila mtanzania tofauti na ilivyo sasa. 

Katika siku yake hii ya kuzaliwa, Mhe. Mbowe ameandika haya katika ukurasa wake wa FACEBOOK (FB); 
“Ndugu zangu wa Watanzania, mimi Mbowe ikiwa leo ni siku yangu ya kuzaliwa ninatimiza miaka 51 sasa, pia ninatimiza miaka 21 nikiongoza siasa za upinzani zenye lengo la kuleta ukombozi wa kweli kwa Taifa hili.
Nimefunguliwa kesi za uchochezi tisa hadi leo, lakini sitaacha harakati hata wakinifunga, bado nitaendelea na harakati za ukombozi hadi Watanzania watakapofikia kwenye uhuru wa kweli,” Ahsante kwa wale wote mnaoendelea kunitakia kheri ya maisha marefu.
Hivyo sisi MaxmillianKattikiro Blog kama wadau wa maendeleo tunapenda kuungana na Mhe. Freeman Mbowe katika kusheherekea siku yake hii ya kuzaliwa na tunampongeza na kumwombea sana ili Mungu mwenyezi azidi kumtia nguvu ya kuwapigania watanzania. 
Vilevile tunamboa afya njema zaidi, Mungu ampatie maisha marefu zaidi, ili ndoto na mipango yake itimie kadri Mungu atakavyomjalia. Watanzania tunamwamini na tuko pamoja naye kusaidiana na kushirikiana katika harakati hizo za ukombozi wa kweli. 
 Mungu akubariki sana. 
 

No comments:

Post a Comment