|  | 
| Mtoto Juliana Mwinuka. | 
Msamaria  mwema mdau wa mtandao huu  
kutoka jijini Dar es Salaam ameungana na  wadau  wa
mtandao (Blog)  wa Francis Godwin kujitolea gharama zote za usafiri
kutoka kijiji cha Mavanga Ludewa hadi jijini Dar es Salaam ili kumwezesha
mtoto  Juliana Mwinuka mkazi wa Mavanga wilaya ya Ludewa  ambaye
amekuwa akitabika nyumbani na majeraha ya  moto kufika Hospitali 
kuanza matibabu  wakati jitihada za mtandao  huu kuendelea
kumchangishia  fedha zinafanyika.
Mdau huyo ametoa kiasi cha shilingi 162,000 kama nauli ya bibi wa mtoto huyo ,mgonjwa mwenyewe na msindikizaji mmoja kutoka Ludewa hadi Dar es Salaam .
Kutokana na jitihada hizo tayari uongozi wa mtandao huo umefanya mikakati ya kufikisha fedha hizo na kumpata kijana Geophrey Katambala wa shirika la Miso ambaye amepatikana kwa msaada wa mwanarahakati Jemida Kulanga ambaye ndie alioweza kufikisha taarifa ya tatizo la mtoto huyo katika mtandao huo .
Hivyo basi mgonjwa huyo leo anatarajia kufika jijini Dar es Salaam Tanzania kwa ajili ya kuanzishiwa matibabu ,wewe kama mdau na msamaria mwema unaombwa kuungana na wadau wengine kunusuru maisha ya mtoto Juliana na pia mtandao huu unawapongeza wote ambao wamenyosha mikono yao na kuchangia kulingana na uwezo wao na Mungu awazidishie daima.
Hawa hapa chini ndio ambao wameanza kuguswa na tatizo la mtoto huyo kwa kuchangia fedha kwa njia ya M-PESA kwa namba 0754 026299 ama Tigo Pesa 0712 750199
Hashimu Mbambo (Tsh. 5,000), Neema Ayoub (Tsh 15,000),Onesmo Lulandala(Tsh 10,000),Gasto Mgeni (Tsh. 20,000)na Allin Allin (Tsh 10,000) na Mussa Ayoub (Tsh 10,000)mmiliki wa mtandao huo wa Francis Godwin kwa niaba ya watanzania wote anapenda kuwapongeza wote walioguswa na tatizo la mtoto Julian Mwinuka na kuwaomba wengine zaidi kujitokeza kuchangia chochote kwa namba hizo hapo juu.
Mdau huyo ametoa kiasi cha shilingi 162,000 kama nauli ya bibi wa mtoto huyo ,mgonjwa mwenyewe na msindikizaji mmoja kutoka Ludewa hadi Dar es Salaam .
Kutokana na jitihada hizo tayari uongozi wa mtandao huo umefanya mikakati ya kufikisha fedha hizo na kumpata kijana Geophrey Katambala wa shirika la Miso ambaye amepatikana kwa msaada wa mwanarahakati Jemida Kulanga ambaye ndie alioweza kufikisha taarifa ya tatizo la mtoto huyo katika mtandao huo .
Hivyo basi mgonjwa huyo leo anatarajia kufika jijini Dar es Salaam Tanzania kwa ajili ya kuanzishiwa matibabu ,wewe kama mdau na msamaria mwema unaombwa kuungana na wadau wengine kunusuru maisha ya mtoto Juliana na pia mtandao huu unawapongeza wote ambao wamenyosha mikono yao na kuchangia kulingana na uwezo wao na Mungu awazidishie daima.
Hawa hapa chini ndio ambao wameanza kuguswa na tatizo la mtoto huyo kwa kuchangia fedha kwa njia ya M-PESA kwa namba 0754 026299 ama Tigo Pesa 0712 750199
Hashimu Mbambo (Tsh. 5,000), Neema Ayoub (Tsh 15,000),Onesmo Lulandala(Tsh 10,000),Gasto Mgeni (Tsh. 20,000)na Allin Allin (Tsh 10,000) na Mussa Ayoub (Tsh 10,000)mmiliki wa mtandao huo wa Francis Godwin kwa niaba ya watanzania wote anapenda kuwapongeza wote walioguswa na tatizo la mtoto Julian Mwinuka na kuwaomba wengine zaidi kujitokeza kuchangia chochote kwa namba hizo hapo juu.
NAWAOMBA TUENDELEE KUCHANGIA FEDHA KWA
AJILI YA MTOTO JULIANA MWINUKA UHAI WAKE UPO MIKONONI MWETU WASAMARIA
WEMA
MAXMILLIAN KATTIKIRO BLOG INAUNGANA NA WADAU WENGINE WOTE KATIKA KUUNGA MKONO JUHUDI HIZI ZA KUMSAIDIA MTOTO JULIANA ILI AWEZE KUPATA MATIBABU NA KUPONA HARAKA. 
MWENYEZI MUNGU AWAZIDISHIE KWA UKARIMU WENU KWANI KUTOA NI MOYO NA SI UTAJIRI!.

 
 
No comments:
Post a Comment