To Chat with me click here

Saturday, September 1, 2012

RAIS JAKAYA KIKWETE ATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MELES ZENAWI, ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO, AWEKA SHADA LA MAUA


Rais  Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo leo  ikulu ya Addis Ababa kufuatia kifo cha Waziri Mkuu wa Ethiopia Marehemu Meles Zenawi anayetarajiwa kuzikwa kesho. Wengine katika picha ni baadhi ya wajumbe waliofuatana na Rais Kikwete watakoshiriki mazishi ya kiongozi huyo.  Kutoka kushoto ni Mbunge wa Mtera Mhe.Livingstone Lusinde, Aliyewahi kuwa balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Jenerali Mirisho Sarakikya, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia Mhe.Joram Boswaro, Mbunge wa Kigoma Kaskazini Mhe.Zitto Kabwe na Waziri wa Kazi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe.Haroun Ali Suleiman.
 Rais  Jakaya Mrisho Kikwete akiweka shada la maua na kutoa heshima zake mwisho kwa aliyekuwa Waziri mkuu wa Ethiopia Marehemu Meles Zenawi katika Ikulu  ya Addis Ababa jioni hii
 
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akito heshima zake mwisho kwa aliyekuwa Waziri mkuu wa Ethiopia Marehemu Meles Zenawi katika ikulu  ya Addis Ababa jioni hii
Rais Dkt.Jakaya Mrisho kikwete akikutana na kufanya mazungumzo na Kaimu Waziri MKuu wa Ethiopia Mhe. Hailemariam Dessalegn jijini Addis Ababa jioni hii.

No comments:

Post a Comment