To Chat with me click here

Thursday, October 25, 2012

UGANDA: MADAI YA UN DHIDI YETU SIO KWELI



Uganda inatishia kujiondoa katika mazungumzo ya kuleta amani katika nchi kadhaa barani Afrika.

Tisho hilo linafuatIa ripoti ya Umoja wa mataifa iliyokashifu Uganda kwa madai ya kuunga mkono makundi ya waasi katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Waziri wa serikali , Asuman Kiyingi, alisema kuwa dhana kuwa Uganda inaunga mkono waasi wa M23 katika DRC wakati ikiwa mpatanishi mkuu katika mazungumzo ya amani ni njama ya kuidhalilisha na kuiharibia sifa nchi hiyo.

Aliongeza kuwa , ikiwa madai hayo hayataondolewa dhidi yake pamoja na juhudi za nchi hiyo kukosa kutambulika, serikali itaondoa wapatanishi wake kwenye mazungumzo ya amani.

Amesema pia vikosi vya nchi hiyo vilivyo nchini Somalia na Jamuhuri ya Afrika ya Kati, pia vitaondolewa.

Vikosi hivyo vinaungwa mkono na Umoja wa Mataifa hatika harakati zao dhidi ya waasi na wanamgambo.

No comments:

Post a Comment