To Chat with me click here

Monday, October 8, 2012

MSIGWA, NASARI KUWAHUTUBIWA WANANCHI UWANJA WA MWEMBETOGWA IRINGA LEO

Iringa Urban Legislator, Hon. Rev. Peter Msigwa

Mbunge wa Jimbo  la Iringa mjini kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mchungaji Peter Msigwa anatarajiwa kufanya mkutano mkubwa leo Iringa.


Akizungumza kwa njia ya simu na mtandao huu Msigwa amesema mkutano huo unatarajiwa kuanza kuanzia saa tisa alasiri katika uwanja wa mwembetogwa.

Amesema kuwa ameamua kufanya mkutano huo ili kuweza kupata maoni toka kwa wananchi kabla ya kurudi bungeni ili aweze kuwasilisha kero zao na kuwa ni njia mojawapo ya kuweka uhusiano mzuri baina ya wananchi hao na mbunge huyo.

Ameongeza kuwa katika mkutano huo atakuwepo mbunge wa Joshua Nasari "Dogo Janja" kwaajili ya kuwapa hamasa vijana kufahamu demokrasia iliyo makini na kila mtu kuitumia katika kufanya maamuzi katika jamii yake.

Amewataka wananchi wa Jimbo la Iringa mjini na vitongoji vyake kujitokeza kwa wingi ili waweze kupata fursa ya kueleza kero zao.

No comments:

Post a Comment