To Chat with me click here

Thursday, October 18, 2012

CCM, CHADEMA WALUMBANA MSIBANI



VIONGOZI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)  katika Wilaya ya Mbeya Mjini juzi waliingia katika malumbano ya kung`ang`ania msiba baada ya kila chama kudai msiba huo unakihusu.

 Katika msiba huo ulikuwa wa  mama mmoja aliyefahamika kuwa ni  RoseMary Mbwete wa eneo la Mwanjelwa, jijini Mbeya.Katika tukio hilo viongozi na wanachama wa vyama hivyo walitoa magari kwa ajili ya matangazo na muziki.

Chadema ndiyo walikuwa  wa kwanza kuwasili na gari lao mapema saa 3:00 asubuhi na kutaka kuhodhi msiba huo.Mvutano huo ulikuja baada ya Chadema kuwazuia viongozi wa CCM waliotaka kulitumia gari lililotolewa na chama hicho kwa ajili ya shughuli za matangazo.

Kitendo hicho kiliwalazimisha CCM  kwenda kuleta gari la kwao na kusababisha eneo hilo kuwa na  magari mawili ya matangazo.

Hali hiyo ilisababisha kutokuwapo kwa maelewano kwa kuwa  magari yote yalikuwa yanatumika kupiga muziki  na matangazo kwa wakati mmoja.

Hali hiyo ilimlazimisha Mtendaji wa Kata ya Ruanda, Elizabeth Kalinga  kuingilia kati na kwamba hayuko tayari kuona amani inavunjika katika eneo hilo.

 Alikitaka kila chama kufuata taratibu, hatua iliyosaidia kurejesha amani na utulivu.Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Chadema wa Wilaya ya Mbeya Mjini, John Mwambigija alisema wao walikwenda msibani na kuweka bendera ya Chadema kwa ajili ya kumfariji mwenzao aliyefiwa na dada yake.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo, marehemu alikuwa kada wa CCM."Unajua sisi Chadema tupo  karibu na jamii na michango tunayotoa ni mikubwa hali inayowatisha CCM ndiyo maana waliamua kutufanyia vurugu," alisema. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake CCM wa  Wilaya ya Mbeya Mjini,  Shija Mwakatundu alisema kitendo cha Chadema kwenda kwenye msiba wa CCM na kuweka bendera zao kinaashiria vurugu na uchonganishi.

No comments:

Post a Comment