To Chat with me click here

Saturday, October 6, 2012

HABARI MPYA KUHUSU MTOTO JULIANA LEO



Habari  za leo kutoka Hospitali ya Muhimbili zinadai hali ya mtoto Juliana Mwinuka kwa  jana na leo imekuwa ya kutia matumaini baada ya kuanza  kula na kunywa dawa na hata kuomba chakula anachokitaka ,pia jicho lake moja  limeanza  kuonyesha dalili ya  kupona huku tatizo kwa  sasa miguu yake hainyoki na yawezekana akaanzishiwa mazoezi  zaidi .hizi ndizo habari mpya  juu ya Juliana Mwinuka.

Mtandao huu wa Maxmillian Kattikiro unaendelea kuwapongeza wote wanaoendelea kuguswa na kuungana na wadau wengine kumchangia fedha za matibabu ,mtoto Juliana kama anavyoonekana akiwa ameunga uso wake kwa moto ni yatima anahitaji msaada wako ili kunusuru maisha yake waweza kutuma mchango wako kwa njia ya M-PESA katika namba hii 0754 026 299 au Tigo Pesa 0712 750199 namba hizi ni za mmiliki wa mtandao wa Francis Godwin

Usikose kuendelea kufuatilia blog hii, ili kuona picha zaidi za maendeleo ya mtoto Juliana. 

No comments:

Post a Comment