To Chat with me click here

Monday, October 15, 2012

"WOMEN IN BALANCE KITCHEN PARTY GALA" KUFANYIKA OKTOBA 21 MWAKA HUU DIAMOND JUBILEE VIP HALL.


Women in Balance Director - Dina Marios

Mkurugenzi wa Women in Balance Dina Marios akizungumza na wageni waalikwa kufafanua hatua ya awali ya maandalizi ya kufanyika kwa tukio la mafunzo ya‘Kitchen Party Gala’  kwa kina mama jinsi ya kuishi ndani ya ndoa ili kujenga familia bora litakalofanyika mnamo tarehe 21 mwezi huu.

Akifafanua zaidi amesema tukio hilo la 4 litakalokuwa la mwisho kwa mwaka huu litakalofanyika kuanzia saa 8 mchana mpaka saa 4 usiku litafanyika katika hali ya ubora zaidi katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Aidha amewataka wanawake kuhudhuria kwa wingi ili waweze kupata faida kwa ajili yao binafsi na kuweza kuwa waalimu bora kwa waume zao jambo litakalosaidia kuepusha migogoro ya mara kwa mara inayopelekea kuvunjia kwa ndoa.

Wadhamini wa Kitchen Party Gala ni TSN Super Market, Sossi, Coca Cola na Clouds Fm.

Mahali:Diamond Jubilee VIP hall Muda:Kuanzia saa nane mchana mpaka saa nne usiku. Kiingilio ni Tsh 30,000 Ukitaka kubook meza ya watu kumi piga namba 0787583132,0716485666 Safarii hii ukiacha wasemaji kuna burudani ya kila aina ukizingatia ni ya mwisho kabisa kwa mwaka huu.Bila kusahau chakula,na vinywaji laini. 

RANGI YA SIKU.
Kwa muda kina dada/mama mmekuwa mkitoa maoni mnataka kushona nguo mtokelezee. Basi rangi ya siku ni rangi ya chenza (tangerine tango)color of the year 2012. Ishone utakavyotaka wewe iwe kitambaa cha kawaida,kitenge,kanga,batiki,au ukachanganya vyovyote ili mradi uzingatie rangi ya siku.

No comments:

Post a Comment