To Chat with me click here

Thursday, October 11, 2012

KAMPUNI YA SHELL YASHTAKIWA NA WANIGERIA

Eneo la Niger Delta lina barabara chache na vijiji vingi havina umeme wala maji safi
Kampuni kubwa ya mafuta ya Shell inatarajiwa kufikishwa mahakamani leo nchini Uholanzi, ikikabiliwa na mashtaka ya kuchafua mazingira katika vijiji kadhaa nchini Nigeria. Kesi hiyo imewasilishwa mahakamani na wakulima wanne wa Nigeria kwa ushirikiano na shirika moja la kutetea mazingira la nchini humo, Friends of the Earth.

Ni mara ya kwanza kwa kampuni kubwa ya Uholanzi inashtakiwa katika mahakama ya kiraia nchini humo kuhusiana na uharibifu uliotokea katika nchi ya kigeni. Shell, inasisitiza kuwa haijaweza kusafisha eneo ambalo lilichafuka kutokana na shughuli zake nchini Nigeria. Inasemekana kuwa nusu ya uvujaji wa mafuta katika eneo hilo imesababishwa na visa vya wizi.

Kesi hiyo inahusishwa na uvujaji wa mafuta uliotokea katika eneo la Ogoniland nchini Nigeria. Wakulima wanasema kuwa mafuta yaliyovuja kutoka kwa mabomba ya mafuta ya kampuni hiyo, yameathiri mapato yao, kwa kuharibu mimea na mabwawa ya samaki.

Mmoja wa walioshtaki kampuni hiyo, Alfred Akpan, aliambia BBC kuwa mafuta yaliyovuja yaliharibu vibaya mabwawa yake 47 ya samaki na anataka fidia.

No comments:

Post a Comment