To Chat with me click here

Saturday, October 13, 2012

VIONGOZI CHADEMA WANASURIKA KUTEKWA



VIONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamenusurika kutekwa baada ya gari lao aina ya Toyota Opa lenye namba za usajili T 850 BLK, kushambuliwa na watu wasiojulikana na kuvunjwa kioo cha nyuma na kitu kizito.

Tukio hilo lilitokea Oktoba 9, mwaka huu majira ya saa nne usiku wakati viongozi hao wakitoka katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani katika Kata ya Mpwapwa Mjini.

Shambulizi dhidi ya viongozi hao waliokuwa katika gari hilo mali ya Eva Mpagama ambaye ni Mratibu wa Vijana CHADEMA Mkoa wa Dodoma, lilifanyika katika eneo la Mwanakianga, nje kidogo ya mji wa Mpwapwa.

Walioshambuliwa ni Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Mafunzo CHADEMA Taifa, Benson Kigaila, Mratibu wa Vijana Mkoa wa Dodoma, Mpagama na Kunti Yusufu ambaye ni mratibu wa akina mama CHADEMA mkoa.

Tukio hilo liliripotiwa Oktoba 10 katika kituo cha polisi cha Wilaya ya Mpwapwa, na kufunguliwa jalada namba RB/1934/2012.

No comments:

Post a Comment