Mbunge
wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (chadema) kesho
kushiriki  mdahalo na   wapiga kura  wake  jimboni kwake
Iringa  katika mwendelezo wa midahalo ya kutathimini haki na
fursa sawa kwa jinsi zote majimboni mwao.
Katika mdahalo huo ulioandaliwa na mtandao  wa mashirika yasiyo ya
kiserikali katika mkoa wa Iringa(ICISO -UMBRELLA) kwa kushirikiana na mitandao
ya AZAKI  ya halmashauri ya manispaa ya Iringa (IMUCISO) na Iringa
Vijijini (IRUNGO) mbunge Msigwa  ambaye ni mbunge wa  jimbo
la  amealikwa  kushiriki mdahalo  huo ambao pia
unaweza  kumshirikisha na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta
Kabati (CCM)
Katibu mtendaji wa ICISO-UMBRELLA Raphael Mtitu alisema kuwa tayari mdahalo huo umefanyika katika jimbo la Kilolo ,Isimani na Kalenga .
Mititu alisema mbali na majimbo hayo mdahalo huo utahitimisha kesho katika ukumbi wa VEta mjini Iringa kwa kumshirikisha mbunge Msigwa .
Katibu mtendaji wa ICISO-UMBRELLA Raphael Mtitu alisema kuwa tayari mdahalo huo umefanyika katika jimbo la Kilolo ,Isimani na Kalenga .
Mititu alisema mbali na majimbo hayo mdahalo huo utahitimisha kesho katika ukumbi wa VEta mjini Iringa kwa kumshirikisha mbunge Msigwa .
Alisema
kuwa   lengo la mdahalo huo ni kuongeza uewelewa kwa wananchi kuhusu
umuhimu wa haki na fursa sawa kwa jinsia katika mkoa wa iringa na wilaya zake
kwa ujumla."lengo ni kuwapa wanajamii uelewa juu ya haki za kijinsia na
kupunguza matukio ya ubaguzi na unyanyasaji wa kijinsia katika ngazi mbalimbali
katika kaya,familia na jamii.

 
 
No comments:
Post a Comment