To Chat with me click here

Thursday, October 25, 2012

UMOJA WA MATAIFA WAITAKA TANZANIA KULINDA MISITU


Climate Change Advisor at United Nations Development Programme, Dr Amani Ngusaru

Mshauri mkuu wa mabadiliko ya hali ya hewa katika Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) Amani Ngusaru aliwataka Watanzania wanaoishi karibu na Msitu wa Pugu kukumbatia mfumo endelevu wa maisha. 

"Mnazo changamoto nyingi zikiwemo kuongezeka kwa uchafuzi wa hali ya hewa, na katika suala hili, maendeleo endelevu ni muhimu na kila mtu analazimika kuyalinda mazingira," Ngusaru alisema, kwa mujibu wa gazeti la The Guardian la Tanzania.

Msitu wa Pugu ni moja ya mfumo wa ikolojia mkongwe kabisa ulimwenguni, ambao ni makazi ya aina 80 za ndege na maji safi ya Mto Msimbazi ambayo yanatoa maji ya kunywa kwa jamii za jirani, alisema, na kuongeza kuwa unahitajika kulindwa kutokana na athari hasi za mabadiliko ya hali ya hewa, kama vile upungufu wa maji, umalizaji wa mfumo wa ikolojia, upatikanaji duni wa nishati na kuenea kwa jangwa. 

Ngusaru aliwataka Watanzania kuangalia katika matumizi ya vyanzo vya nishati mbadala na majiko ya kupikia ya kuokoa nishati ili kusaidia juhudi za serikali za kupunguza athari za mabadiliko ya hali ya hewa na kuboresha shughuli za maendeleo endelevu.

No comments:

Post a Comment