To Chat with me click here

Tuesday, October 23, 2012

TANZANIA YAKATAA KUJIHUSISHA NA PEMBE ZA NDOVU ZILIZOKAMATWA


Pembe za ndovu zilizokamatwa katika operesheni dhidi ya biashara ya magendo huko Hong Kong zikioneshwa kwenye mkutano wa vyombo vya habari hapo tarehe 20 Oktoba.  

************************************
Viongozi wa Tanzania wakataa kuhusika na tani 3.18 pembe za ndovu za magendo zilizokamatwa huko Hong Kong mwishoni mwa wiki, wakidai kuwa idadi kubwa kama hiyo ya pembe za ndovu haiwezekani kuwa zimetoka nchini kwao, gazeti la Daily News la Tanzania liliripoti siku ya Jumatatu (tarehe 22 Oktoba). 


Viongozi wa Hong Kong walisema kuwa pembe hizo zilikuwa zimesafirishwa kutoka Kenya na Tanzania na zilikuwa na thamani ya zaidi ya dola milioni 3.4

"Tanzania imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuzuwia uwindaji haramu wa tembo na wanyama wengine wa msituni," alisema Paul Sarakikya, afisa wa wanyamapori katika Wizara ya Maliasili na Utalii ya Tanzania. "Inaweza kutokea kwa kesi adimu sana, lakini kiwango kikubwa kama hicho cha pembe za ndovu haziwezi kuwa zimekusanywa kutoka nchini." 

Sarakikya alisema kuwa wawindaji haramu wanaofanya kazi hiyo katika nchi zisizo bahari kama vile Zambia, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo au Mozambiki hutumia bandari ya Dar es Salaam kusafirisha bidhaa zao, na kuongeza kuwa bandari inapaswa kufanya upekuzi zaidi wa makontena yanayotoka nje ili kuzuwia biashara haramu ya pembe za ndovu. 

Hivi karibuni Tanzania iliomba idhini kutoka kwa Makubaliano ya Kimataifa juu ya Biashara ya Kimataifa ya Wanyama Walio Hatarini ili kuuza baadhi ya lundiko la pembe zake za ndovu, zenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 87.8 (dola milioni 55.5).

 

No comments:

Post a Comment