To Chat with me click here

Tuesday, October 9, 2012

MNYIKA: CCM NI JANGA



MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), amewataka Watanzania kukichukulia Chama cha Mapinduzi (CCM) na kukiona kama janga la kitaifa kwani kimeshindwa kutatua matatizo yao.

Kauli hiyo aliitoa juzi wakati wa uzinduzi wa kampeni ya uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya Msalato, manispaa ya Dodoma.

Mnyika alisena kuwa CCM imechangia kwa kiasi kikubwa kuwadidimiza Watanzania kutokana na kushindwa kusimamaia rasilimali zilizopo na kuwaruhusu wageni kuzitumia bila kuwashirikisha Watanzania.

Alisema kuwa Watanzania wengi wamekuwa maskini katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru wakati kuna wachache ambao wanamiliki fedha nyingi. CHADEMA wamemsimamisha Nsubi Bukuku kuwa mgombea udiwani katika kata hiyo.

Naye Afisa Habari wa CHADEMA, Tumaini Makene, alisema vurugu zilizotokea juzi kabla ya mkutano wao juzi zilisababishwa na wanachama wa CCM kuvamia msafara wao.

Majeruhi katika vurugu hizo ni Katibu wa UVCCM wa kata ya Kiwanja cha Ndege, Ali Swalehe; mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji wa CCM Dodoma Mjini, Fatma Mwihidini; Diwani wa kata ya Uhuru, Ali Kimaro; Hussein Mtengule na Waziri Shabani.

Hata hivyo, habari hizo zilisema kuwa hakuna mtu anayeshikiliwa na polisi kuhusiana tukio hilo hadi sasa. Kamanda wa polisi mkoani hapa, Stephen Zelothe, alipoulizwa kuhusiana na vurugu hizo alisema yuko safarini kurejea mjini Dodoma na kwamba angetoa taarifa kwa waandishi atakapofika.

No comments:

Post a Comment