Serikali
yetu  ni bingwa sana katika kuzungumza ila si katika utendaji huu ni
uwanja  wa ndege  wa muda sana hapa mkoani Iringa  lakini
gari  linalotumika kwa ajili ya kuzima uokoaji katika uwanja  huo ni
kituko kama ambavyo unaona pichani .
Mbali
ya wizara hiyo ya uchukuzi  kuendelea  kubadilishwa mawaziri na
manaibu wake kila wakati ila hakuna jipya ambalo  wamekuwa wakilifanya kwa
uwanja huu ambao ni tegemeo katika mkoa wa Iringa hasa ukizingatia kuwa
mawaziri hao, manaibu na viongozi wa serikali ngazi ya mkoa na wilaya 
wamekuwa wakibadilisha magari kila wakati huku  wakisahau kuwa uwanja huo
ndio wao  wamekuwa wakiutumia pindi  wanapokuja Iringa sasa ikitokea
ajali ni  wa kwanza kuunda tume za kuchunguza chanazo cha ajali.
Nini
maoni yako mdau  wa mtanado  huu juu ya uwanja  huu wa Nduli
Iringa?

 
 
No comments:
Post a Comment