To Chat with me click here

Tuesday, October 9, 2012

HILI NDILO GARI PEKEE LA ZIMAMOTO KATIKA UWANJA WA NDULI IRINGA .....




Serikali yetu  ni bingwa sana katika kuzungumza ila si katika utendaji huu ni uwanja  wa ndege  wa muda sana hapa mkoani Iringa  lakini gari  linalotumika kwa ajili ya kuzima uokoaji katika uwanja  huo ni kituko kama ambavyo unaona pichani .

Mbali ya wizara hiyo ya uchukuzi  kuendelea  kubadilishwa mawaziri na manaibu wake kila wakati ila hakuna jipya ambalo  wamekuwa wakilifanya kwa uwanja huu ambao ni tegemeo katika mkoa wa Iringa hasa ukizingatia kuwa mawaziri hao, manaibu na viongozi wa serikali ngazi ya mkoa na wilaya  wamekuwa wakibadilisha magari kila wakati huku  wakisahau kuwa uwanja huo ndio wao  wamekuwa wakiutumia pindi  wanapokuja Iringa sasa ikitokea ajali ni  wa kwanza kuunda tume za kuchunguza chanazo cha ajali.

Nini maoni yako mdau  wa mtanado  huu juu ya uwanja  huu wa Nduli Iringa?

No comments:

Post a Comment