To Chat with me click here

Wednesday, August 8, 2012

RAIS KIKWETE AREJEA NYUMBANI BAADA YA KUHUDHURIA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI ZA MAZIWA MAKUU


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Mwenyekiti wa Mkutano wa wakuu wa nchi za Maziwa Makuu,Rais Yower Kaguta Museveni wa Uganda mwishoni mwa mkutano huo uliomalizika leo jijini Kampala Uganda.

 Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitia saini maazimio ya wakuu wa nchi za Maziwa Makuu mwishoni mwa mkutano huo uliofanyika katika Hoteli ya Speke’s Bay Resort,Munyonyo, KAMPALA, Uganda.

Waziri wa Mambo ya nje Bernard Membe na Meya wa Jiji la Dar es Salaam Dkt. Didas Masaburi wakimkaribisha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere akitokea jijini Kampala Uganda ambapo alihudhuria mkutano wa wakuu wan chi za Maziwa Makuu.

No comments:

Post a Comment