Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Morogoro, Faustine Shilogile.
WAKATI
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kikitarajia kufanya mkutano mkubwa
mjini Morogoro kuhitimisha operesheni yake ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C)
iliyodumu kwa wiki tatu, Jeshi la Polisi mkoani hapa limejiingiza tena kwenye
msuguano na chama hicho.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, amewakatalia CHADEMA kufanya
maandamano wakati wakielekea kwenye uwanja wa mkutano wao leo katika viwanja
vya Shule ya Msingi Kiwanja cha Ndege na kuwashirikisha viongozi wa juu wa
chama hicho.
Agosti
4, mwaka huu, Kamanda Shilogile alizua tafrani wakati CHADEMA wakianza mikutano
yao mkiani hapa, baada ya kuizuia akidai hawana askari wa kutosha kwani
maonesho ya wakulima Nanenane yalikuwa yakiendelea.
Hata
hivyo, maelezo hayo yalipingwa vikali na viongozi wakuu wa CHADEMA na
kushinikiza kufanya mikutano hiyo kwa nguvu kwani ilikuwa imeruhusiwa kihalali
na jeshi hilo, jambo lililosababisha kufanyika majadiliano baina ya pande hizo
na muafaka kupatikana.
Lakini
katika hatua inayoonesha kama kutaka kuibua upya msuguano huo, jana Kamanda
Shilogile, alieleza sababu za kuzuia maandamano hayo kuwa ni udogo wa barabara
za mji wa Morogoro, na kwamba leo ni siku ya kazi, hivyo yanaweza kuleta
usumbufu kwa wananchi.
Wakati
Shilogile akitoa kauli hiyo, Mkuu wa Operesheni Sangara, Benson Kigaila,
alisema watafanya maandamano hayo kwa vile walishakubaliana na jeshi hilo kabla
ya kuwageuka.
Badala
yake Shilogile alisema wataruhusu watu wasiozidi 50 kupita kwa wakati mmoja
pasipo kuwa na ishara ya kuonesha kama wanaelekea katika maandamano.
“Sisi
tumewaambia viongozi wao watapanda magari, lakini wananchi watafute njia ya
kufika huko na si kwa maandamano, hilo hatuwezi kuruhusu,” alisema Shilogile.
Alipoulizwa
makubaliano yaliyofikiwa awali baina yao na CHADEMA juu ya kupanga njia ya
kupita kwa maandamano hayo, Shilogile alisema hakukuwa na makubaliano ya namna
hiyo.
Hata
hivyo, Kigaila alisema wanachojua wao ni kwamba mikutano yao ipo kisheria, na
kwamba wameshatoa taarifa kama inavyotakiwa hata kufikia hatua ya kukubaliana
kwenda kupanga njia ya kupita.
Alisema
sababu alizotoa Shilogile hazina mashiko kwa kuwa barabara za Morogoro ni sawa
na za miji mingine, na kwamba ndani ya mkoa huo kulishafanyika maandamano
mengine tofauti na ya CHADEMA.
No comments:
Post a Comment