To Chat with me click here

Friday, August 31, 2012

MCHUNGAJI ,MBUNGE NA DR. GETRUDE RWAKATARE AFUNGUA JENGO LAKE JIPYA JIJINI DAR ES SALAAM

Muonekano wake kwa nje.
MC na mchungaji Haris Kapiga wa Clouds FM
  Mc Harris Kapiga akiwa kazini.
 Kabati la vyombo
 Akiwa katika ofisi yake ya nyumbani, kuna sehemu ya kufanyia mikutano,Salon,Studio,na sehemu ya mazoezi.
  Ukifika wakati wa misosi kwa wageni.
Midundo na burudani zilitawala, namwona Veronica Joseph akiwa amepiga pamba ya blue
  Chumbani sehemu ya kujipamba.
 Kitanda chake cha kulala

Nimeamini kuwa ukifanya kazi ya Mungu kwa uaminifu naye atakulipa hapa hapa dunia, na utakuwa ushuhuda kwa watu wengine. Mama Getrude Rwakatre siku ya Jumapili alikuwa anahamia rasmi katika nyumba yake mpya iliyoko Mbezi Beach jijini Dar es Salaam pembezoni mwa bahari ya Hindi. Waumini wa kanisa hilo wapatao takribani 300 walifika mahali hapo kwa kushuhudia nyumba ya kifahali.

Mch. Mh. Getrude Pangalile Rwakatare kabla ya kuhamia kwenye hekalu lake jipya alikuwa akiishi Mikocheni B katika nyumba ya kifahali pia. Alizidi kukaa katika uwepo wa Mungu na kufanya kazi yake kwa bidii na kujituma. Katika mahubiri yake kwa waumini wake amekuwa akiwatabiria watu mafanikio na watu wamefanikiwa kutokana na utabiri wake. Leo hii imekuwa zamu kwake ambapo Mungu hakutaka kumuaibisha kama mtumishi wake, akamshangaza kwa muujiza wa kumuwezesha kujenga jumba la kifahari kwa gaharama kubwa sana,

Nisowachoshe kwa maneno mengi, naomba tuangalie kazi ya Mungu kwa wanadamu.

Habari kwa hisani ya Riziki Mgaya.

No comments:

Post a Comment