To Chat with me click here

Thursday, August 30, 2012

HONGERA SANA THEOPISTA SANGA.


Theopista F. N. Sanga
Ilikuwa siku kama ya leo miaka tisa (9) iliyopita katika kanisa la Mt. Joseph, jimbo kuu la Dar-es-Salaam, ambapo mpendwa wetu Theopista F. Nsanzugwanko na Ndg. Deus Sanga walifunga ndoa. 

Kama kila mmoja wetu afahamuvyo juu ya maisha ya ndoa hujawa na misukosuko mingi ya kimaisha, majaribu, shida za kiuchumi na makandokando mengi, halikadharika ndoa ya Theopista nayo haikukoswa na magumu hayo ya kimaisha. 

Lakini kwakuwa Theopista Nsanzugwanko, alilelewa katika familia ya kikristo ambayo mkuu wa familia hiyo Hayati Baba Firdbety Nsanzugwanko (Mungu amlaze mahali pema peponi) alikuwa ni mtumishi mwema wa Mungu, hakusita kuwaongoza watoto wake akiwemo yeye (Theo) katika misingi mizuri ya kidini, akiwafundisha kuwa WAVUMILIVU, WANYEYEKEVU, WENYE KUELEWA WENGINE na WENYE KUMWAMINI NA KUMCHA MUNGU. 

Kutokana na mafundisho hayo mema ya mzee wao, ndugu yetu Theo ameweza kuvumilia mengi mno katika kipindi hicho chote cha maisha yake ya ndoa. Hivi sasa Mungu amembariki na watoto wawili Witness Sanga (Mke) na Winston Sanga (Mme). Pia katika majaribu na magumu yote, mama huyu wa watoto wawili ameweza kumudu kuwasomesha watoto wake wote wawili, yeye mwenyewe kujiendeleza, pia kusimamia mambo muhimu ya kuimarisha familia yao kama ujenzi wa nyumba na mengine mengi, kwa msaada mkubwa wa mumewe ndg. Deus Sanga pamoja na Mungu akiwaongoza. 

Siri kubwa ya mafanikio ya Theo katika ndoa yake, ni uchaji na uvumilivu alionao, ambao wanawake wengi na wadada wa kileo wamekuwa hawana sifa hii ya uvumilivu. Ni vyema wanawake wakaiga tabia hii ya Theopista na kujiepusha na tamaa za kupata maendeleo ya haraka haraka ambazo huweza kuharibu maisha yao ya ndoa. 

Katika kusherehekea siku hii kubwa ya ndoa yake, Theopista ameandika haya kwenye kurasa zake za facebook kwa marafiki zake;
mungu ni mwema ukimtumaini sina neno kubwa la kumshukuru bali nikusema aksante kwa upendo wake kwa familia hii,friends leo ni annivesary ya ndoa yetu mm na my lovely husband Deus Sanga kwani siku kama ya leo miaka kenda iliyopita tulifunga ndoa katika kanisa la mt joseph dsm na tunamshukuru mungu kwa zawadi ya Witness na Winston ehee mungu naomba endelea kupigania ndoa hii upendo na amani vitawale siku zote
Kwakweli, Maxmillian Kattikiro Blog, inapenda kumpongeza sana Theopista kwa mafanikio ambayo ameyapata na pia tunamwombea kwa Mungu azidi kumbariki na kumpitisha salama kwenye njia zake na hivyo siku moja aweze kufanya anniversary ya miaka 100 ya ndoa yake.  
Happy Anniversary Theopista & Deus Sanga.

No comments:

Post a Comment