To Chat with me click here

Saturday, September 29, 2012

MPASUKO WA CCM UMEANZISHWA NA NEC DODOMA, TUSUBIRI JAZBA ZA WALIOTEMWA


HALMASHAURI Kuu ya CCM (NEC), imetangaza majina ya wagombea walioteuliwa kuwania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho, huku ikionyesha kuwa uchaguzi huo utakuwa na mchuano mkali.
Katika orodha iliyotolewa jana, baadhi ya makada wake maarufu akiwamo Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono na Salum Londa wametupwa.

Mchuano mkali unaonekana kuwapo kwenye nafasi ya ujumbe wa Nec Mkoa wa Manyara ambako Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye anachuana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk Mary Nagu.

Mchuano huo unatarajiwa kuwa mkali katika nafasi ya uenyekiti kwenye baadhi ya mikoa kutokana na kupitishwa kwa majina ya makada wake maarufu. Mwanza ni miongoni mwa mikoa hiyo kwani Nec imepitisha jina la Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii, Anthony Diallo ambaye atachuana na Clement Mabina anayetetea nafasi hiyo.

Makada hao watapata ushindani mkali kutoka kwa Zebedayo Athumani, Joseph Yaredi na Mashimba Hussein Mashimba.

Dar es Salaam nako kunatarajiwa kuwa na mchuano mkali kwani mwenyekiti wa sasa, John Guninita atachuana na Mkuu wa Kitengo cha Uchaguzi Makao Makuu ya CCM, Matson Chizzi na kada mwingine, Ramadhan Madabida. Godfrey Mwalusamba, Harold Adamson na Paul Laizer wanawania nafasi hiyo mkoani Arusha.

Katika Jumuiya ya Wanawake wa Tanzania (UWT), ambako Mwenyekiti wa sasa, Sofia Simba ambaye pia ni Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto anachuana na Mbunge wa Same Mashariki, Anna Kilango Malecela na Mbunge wa Viti Maalumu, Mayrose Majige.

NASSARI ASIKILIZA KERO ZA WANANCHI ARUMERU

Nassari MB akiwa na Jackson Makalla (chini kushoto mwenye Kombati) walipokuwa Ngarenanyuki jana
 Nassari akihutubia na kusikiliza maswali ya wananchia

JINSI ILIVYOKUWA KATIKA ZOEZI LA KUMWAGWA JEN. KAMAZIMA



Dk. Edward Hosea ametoa salam za rambi rambi kwa niaba ya Takukuru; Anasema: Marehemu, alihamishiwa TAKURU 1990... Akitokea JWTZ... Hadi anastaafu 2003

WALIOTOSWA CCM WAFICHUA SIRI

FILIKUNJOMBE ADAI YEYE, MKONO, LUGOLA WALIPONZWA NA PINDA, NAPE ATAKA WASIORIDHIKA WAKATE RUFAA, WASOMI WAPONGEZA 

SIKU moja baada ya Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), kutangaza majina ya wagombea, baadhi ya vigogo walioachwa kwenye uteuzi huo wameeleza ya moyoni, huku Mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe akisema anaamini ametoswa kwa sababu alitia saini ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Katika Bunge la 10 lililoketi Aprili mwaka huu, baadhi ya Wabunge wa CCM akiwamo Filikunjombe, Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono na Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola, waliunga mkono hoja ya kutokuwa na imani na Pinda iliyokuwa imeanzishwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe wa Chadema. 

Wabunge hao wa chama tawala, waliungana na wenzao wa upinzani kutaka kupiga kura za kutokuwa na imani na Pinda kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ameshindwa kuisimamia Serikali kwa kuwawajibisha mawaziri wazembe. Hata hivyo, mpango huo haukufanikiwa baada ya Spika wa Bunge Anne Makinda kueleza kuwa haukufuata taratibu zinazotakiwa.
 

 Filikunjombe alipotakiwa jana kuzungumzia kuenguliwa kwake kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi wa ndani ya chama, alisema anaamini yeye na wenzake hao wa CCM, wametoswa kwa sababu ya kushiriki mpango wa kumng'oa Waziri Mkuu Pinda. Hata hivyo, alisema amelazimika kukubali hali hiyo na kupokea matokeo, kwa kuwa hatua yake ya kusaini kitabu hicho ilitokana na nia njema kutaka Waziri Mkuu ajiuzulu ili mambo fulani muhimu katika jamii yafanyike. 

ZITTO: NARUDIA, MWAKA 2015 SITAGOMBEA UBUNGE.


Narudia, mwaka 2015 sitagombea Ubunge. Nitafanya kampeni ya Urais, ama mimi kama mgombea wa chama changu CHADEMA au kama mpiga debe wa mgombea wa chama changu. Miaka 10 ya Ubunge inatosha na kwa ngazi hiyo ni vema niwaachie wengine wasukume mbele gurudumu la maendeleo ya Jimbo na mkoa wetu. Huu ndio uamuzi wangu wa mwisho na nimeshawaeleza wananchi wa Jimbo langu na mkoa wa Kigoma toka mwaka 2005. 

(Inatoka kwenye ukurasa wake wa Face Book)

CCM WASHINDA KITI CHA UMEYA JIJI LA MWANZA.


Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus Mabula kupitia CCM (katikati) akiwa na Naibu Meya John Minja (CCM) wakitambulishwa na Mkurugenzi wa jiji la Mwanza Wilson Kabwe baada ya kutangazwa washindi  kufuatia uchaguzi uliofanyika leo katika ukumbi wa halmashauri ya jiji la Mwanza.

*******************************************

Hatimaye kile kitendawili cha nani atakuwa meya wa jiji la mwanza kati ya vyama viwili vikuu vyenye upinzani mkubwa CCM na CHADEMA kimeteguliwa baada ya chama cha mapinduzi CCM kushinda uchaguzi huo na kutwaa kiti hicho cha umeya wa jiji la mwanza.

Akitangaza matokeo mara baada ya madiwani kupiga kura Mkurugenzi wa jiji la mwanza kabwe amemtangaza Stansilaus Mabula diwani wa kata ya mkolani kuwa meya wa jiji la mwanza baada ya kupata kura 11 na kumwaga chini mpinzani wake kutoka CHADEMA Charless chinchibela aliyepata kura 8.

Nafasi nyingine iliyokuwa ikiwania katika uchaguzi huo ni nafasi ya Naibu Meya wa jiji hilo ambapo Daudi Mkama kutoka CUF kura 8 na John Minja aliyepata kura 10 na kutangazwa rasmi John Minja diwani wa kata ya mbungani kuwa Naibu meya wa jiji lamwanza.

Mara baada ya kutangazwa kuwa meya Mabula ametaka umoja na ushilikiano kutoka kwa madiwani ili kuweza kuwatumikia wananchi kwa nguvu ili kuweza kuwaletea maendeleo na kuliletea sifa jiji la mwanza.

Katibu wa itikadi na uenezi CCM taifa Nape nauye mara baada ya uchaguzi kuisha akajitokeza mbele ya waandishi wa habari kuwapongeza madiwani wa cccm waliochaguliwa kwa nafasi za meya na naibu meya kwa kiuweza kulililudisha jiji la mwanza mikononi mwa ccm.

Amesema kuwa kikubwa ni ushilikiano katika kutenda kazi za wananchi wa jiji la mwanza ili kuweza kuwaletea maendeleo kwa pamoja na kutoa ushilikiano kwa chama cha mapinduzi ili kudumisha umoja na mshikamano.

“Dk. Slaa mara baada ya kuona maji yamemfika shingoni ameamua kutofika katika uchaguzi huu na alikuwa anajua ni jinsi gani uchaguzi utakavyo kuwa na sasa anahamini ya kuwa ccm sio chama cha vurugu kama chama chao na hatuwezi kuongoza kibabe kama wao wananvyozani na tena ninadhani kuwa chadema wameona mavuno ya ubabe wao kuwa hayana umuhimu wowote”. Alisema Nape.

Amesema kuwa ni vyema sasa wanamwanza wakawa na mshikamano na kuacha kufanya maandamano ambayo hayana umuhimu wowote kwao na badala yake wafanye maendeleo na kukaa kwa amani.

 Ni picha ya pamoja Meya Mabula, mkuu wa wilaya ya Nyamagana Baraka Konisaga(katikati) na Naibu meya John Minja wakiwa katika ofisi ya Mstahiki Meya.
Kutoka kushoto ni aliyekuwa Meya wa jiji la Mwanza kabla ya jiji hilo kugawanywa kuwa Manispaa na Halmashauri, diwani Manyarere akiwa na diwani Rose Brown na diwani wa viti maalum ndani ya ukumbi wa Uchaguzi kutafuta Meya na Naibu wake Nyamagana.
 Meya wa jiji la Mwanza (wa3kutoka kushoto) Naibu Meya (wa kwanza kushoto) wakiwa pamoja na Madiwani wa CCM wakimsikiliza mbunge wa viti maalum Maria Hewa (wa pili kutoka kulia) aliyekuwa akisema “Chama kimerudisha heshima yake katika jiji la Mwanza”.

Friday, September 28, 2012

CCM WAIBUKA KIDEDEA UCHAGUZI WA KUMTAFUTA MEYA NYAMAGANA

Kikao cha Uchaguzi cha Halmashauri ya Manispaa ya Nyamagana Jijini Mwanza kimemchagua diwani wa Kata ya Mkolani Mh. Stanslaus Mabula wa CCM kuwa Meya wa Jiji hilo mara baada ya kumshinda mshindani wake Charles Chinchibela wa CHADEMA aliyepata kura 8 ili hali Mabula akipata kura 11.

Tutawaletea taarifa kamili baadaye kidogo, endelea kufuatilia blog hii....

VULLU (CCM) AKALIA KUTI KAVU

NI ANAYEDAIWA KUKAMATWA KWA RUSHWA KISARAWE, NAPE ASEMA ATACHUNGUZWA NA KAMATI YA MAADILI

Hon. Zaynab Vullu (CCM) Special Sit
MBUNGE wa Viti Maalum, Zainab Vullu (CCM), Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), Wilaya ya Kisarawe, Asia Madima na Katibu wa UWT wa wilaya hiyo, Mwajuma Mombwe, wako hatarini kung’olewa katika nafasi wanazogombea.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, jana alisema kwamba baada ya vyombo vya habari kuripoti jana, kwamba Vullu na wenzake hao walikamatwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Wilaya ya Kisarawe, Kamati ya Maadili ya CCM itakwenda Kisarawe kuchunguza tuhuma hizo.

Kwa mujibu wa Nape, kama kamati hiyo ikithibitisha kwamba Vullu, Asia na Mwajuma walikamatwa wakigawa rushwa, wataondolewa mara moja kwenye mchakato wa kugombea nafasi mbalimbali za chama hicho.

Vullu ndiye Mwenyekiti wa UWT Mkoa wa Pwani na anatetea nafasi yake.
“Mgombea yeyote atakayebainika kukiuka maadili kwa kutoa rushwa katika chaguzi mbalimbali zinazoendelea ndani ya chama, ataondolewa kwenye mchakato wa uchaguzi.

“Nasema hivyo kwa sababu majina ya wanachama yaliyopitishwa katika vikao vya chama hayamaanishi kwamba wagombea wamehakikishiwa ushindi wa kufanya watakavyo.

“Chama hakitasita kumwondoa mwanachama yeyote atakayebainika kujihusisha na vitendo vya rushwa wakati huu wa mchakato ndani ya chama.

“Sasa nasema hivi, Kamati ya Maadili itakwenda huko Kisarawe kuchunguza tuhuma hizo na kama ikibainika wanachama hao wamejihusisha na vitendo vya rushwa, wataondolewa mara moja kwenye mchakato wa uchaguzi.

“Ni juzi tu Halmashauri Kuu imeonya wote wanaodhani kwamba kupitishwa kwa majina yao katika vikao vya Halmashauri Kuu ni tiketi ya kufanya watakavyo, wanajidanganya.

“Kupitishwa majina yao ni jambo moja na kushiriki mchakato wa uchaguzi ni suala jingine, hivyo wakibainika kukiuka maadili, nasema wataondolewa mara moja kwenye mchakato,” alisema Nape kwa kifupi.

Juzi TAKUKURU, Wilaya ya Kisarawe, Mkoa wa Pwani, iliwatia mbaroni Mbunge wa Viti Maalum, Zainab Vullu (CCM), Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT), Wilaya ya Kisarawe ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Asia Madima, pamoja na Katibu wa UWT wa wilaya hiyo, Mwajuma Mombwe, kwa tuhuma za rushwa.

Chanzo chetu cha habari kilichopo wilayani Kisarawe kilisema kuwa, Vullu na wenzake hao, walikamatwa Jumanne wiki hii, saa 12 jioni, baada ya kudaiwa kugawa fedha kwa wajumbe waliohudhuria kikao cha Baraza la UWT, Wilaya ya Kisarawe, kilichokuwa kikifanyika makao makuu ya CCM, Wilaya ya Kisarawe.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, Vullu, Asia na Mwajuma, walikamatwa na Kamanda wa TAKUKURU, Wilaya ya Kisarawe, aliyetajwa kwa jina moja la Noel.