To Chat with me click here

Friday, August 31, 2012

CCM YAFIKA PABAYA


DK. KIGWANGALA, BASHE WATISHIANA BASTOLA NZEGA

KATIKA kile kinachoonekana kama vita ya urais wa mwaka 2015, makundi yanayokinzana ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), yamedaiwa kuanza mkakati wa kujiimarisha kwa kutumia uchaguzi wa ndani unaoendelea sasa.

Hatua hiyo vile vile inaelezwa kuwa ni mwendelezo wa visasi vya Uchaguzi Mkuu uliopita katika baadhi ya maeneo, ambapo wagombea wanaokubalika waliachwa na kuchukuliwa wengine.

Mathalani katika Jimbo la Nzega, mkoani Tabora, visasi hivyo vimedumu baina ya Mbunge wa sasa, Dk. Hamis Kigwangala na kada aliyeenguliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa, Hussein Bashe, akidaiwa si raia wa Tanzania.

Wawili hawa juzi wanadaiwa kutishiana bastola katika ofisi ya CCM wilayani humo wakati wakirejesha fomu za kuomba kuwania nafasi mbalimbali.

Taarifa kutoka vyanzo vyetu vya ndani ya chama hicho, zinaeleza kuwa miongoni mwa vigogo wanaotajwa kuutaka urais, makundi ya Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa na lile la Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe, ndiyo yanamsuguano mkali.

KITU CHALI!!!



Hii imetokea kitambo kidogo maeneo ya Mbezi mwisho (Mbezi ya Ubungo) ktk harakati za kupanua barabara kwa ajili ya magari yaendayo kwa kasi.Picha kwa hisani ya Mdau.

GAVANA WA BENKI KUU, AZINDUA MFUMO WA KUNUNUA DHAMANA NA HATI FUNGANI KWA NJIA YA MTANDANO


GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu akiongea na waandishi wa habari  jijini Dar es salaam kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo mfumo wa mawakala wa Benki hiyo wa kununua dhamana za Serikali na hati fungani kwa njia ya mtandano(online) kwenye mnada na hivyo kupunguza ule utaratibu wa dhamana wa kupeleka karatasi katika Benki ili kupata huduma hiyo.

Maswali--- GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu(kushoto) na Naibu Gavana wa BoT, Dk Natu Mwamba(kulia) wakinukuu maswali mbalimbali ya waandishi wa habari jana (leo) jijini Dar es salaam kabla hawajaanza kuyatolea ufafanuzi.

MCHUNGAJI ,MBUNGE NA DR. GETRUDE RWAKATARE AFUNGUA JENGO LAKE JIPYA JIJINI DAR ES SALAAM

Muonekano wake kwa nje.
MC na mchungaji Haris Kapiga wa Clouds FM
  Mc Harris Kapiga akiwa kazini.
 Kabati la vyombo
 Akiwa katika ofisi yake ya nyumbani, kuna sehemu ya kufanyia mikutano,Salon,Studio,na sehemu ya mazoezi.
  Ukifika wakati wa misosi kwa wageni.
Midundo na burudani zilitawala, namwona Veronica Joseph akiwa amepiga pamba ya blue
  Chumbani sehemu ya kujipamba.
 Kitanda chake cha kulala

Nimeamini kuwa ukifanya kazi ya Mungu kwa uaminifu naye atakulipa hapa hapa dunia, na utakuwa ushuhuda kwa watu wengine. Mama Getrude Rwakatre siku ya Jumapili alikuwa anahamia rasmi katika nyumba yake mpya iliyoko Mbezi Beach jijini Dar es Salaam pembezoni mwa bahari ya Hindi. Waumini wa kanisa hilo wapatao takribani 300 walifika mahali hapo kwa kushuhudia nyumba ya kifahali.

Mch. Mh. Getrude Pangalile Rwakatare kabla ya kuhamia kwenye hekalu lake jipya alikuwa akiishi Mikocheni B katika nyumba ya kifahali pia. Alizidi kukaa katika uwepo wa Mungu na kufanya kazi yake kwa bidii na kujituma. Katika mahubiri yake kwa waumini wake amekuwa akiwatabiria watu mafanikio na watu wamefanikiwa kutokana na utabiri wake. Leo hii imekuwa zamu kwake ambapo Mungu hakutaka kumuaibisha kama mtumishi wake, akamshangaza kwa muujiza wa kumuwezesha kujenga jumba la kifahari kwa gaharama kubwa sana,

Nisowachoshe kwa maneno mengi, naomba tuangalie kazi ya Mungu kwa wanadamu.

Habari kwa hisani ya Riziki Mgaya.

POLISI WAKARIBISHA M4C


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP), Michael Kamuhanda, amesema hawatakuwa na sababu ya kuzuia mikutano ya CHADEMA baada ya shughuli za sensa kumalizika.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamuhanda alisema tangu siku ya kwanza CHADEMA walipoingia mkoani humo hali ya utulivu ilikuwa ni nzuri na hakukuwa na matatizo yoyote mabaya waliyosababisha.

“Tunajua watafanya mkutano wao Septemba 2, mwaka huu, wilayani Mufindi, hatuna sababu ya kuzuia hilo labda ijitokeza sababu ya kiusalama, kwa kuwa hata Dk. Slaa nimezungumza naye na akaniambia wako salama na amefurahia walivyopokewa kifalme katika mkoa huu,” alisema Kamuhanda.

Akizungumzia sababu ya kuimarisha ulinzi, Kamanda Kamuhanda alisema hatua hiyo inatokana na hali halisi ya kisiasa kwa sasa na kwamba polisi wana wajibu wa kuchukua tahadhari kuhakikisha usalama unakuwepo.

Alipoulizwa kama jeshi hilo linatumiwa na viongozi wa CCM katika kuhakikisha mikutano ya CHADEMA haifanikiwi, Kamuhanda alisema si kweli kwani hata baadhi ya viongozi wa CCM wakiwamo wabunge wa mkoa huo hajawahi kukutana nao.

Tangu kuingia kwa viongozi kadhaa wa CHADEMA mkoani Iringa, jeshi hilo limekuwa katika tahadhari kubwa kwa hofu kuwa wanaweza kufanya mikutano kabla ya sensa ya watu na makazi kumalizika.

DK SLAA AMVUTIA PUMZI SAMUEL SITTA

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amesema kauli iliyotolewa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ni nzito, hivyo anajipanga kuijibu.

Dk Slaa aliliambia gazeti hili jana kuwa asingependa kuzungumzia kauli hiyo sasa kwa kuwa yuko ziarani vijijini, lakini ataitolea tamko wakati mwafaka ukifika.Habari ambazo baadaye gazeti hili lilizitapa zinasema kuwa Dk Slaa huenda akamjibu Sitta leo, atakapokutana na waandishi wa habari mjini Iringa.

Dk Slaa mwenyewe jana jioni alithibitisha kwamba atakutana na waandishi wa habari leo mjini Iringa, lakini hakuwa tayari kueleza kama atazungumzia kauli ya Sitta au la.

Kauli ya Dk Slaa imekuja baada ya gazeti hili kumtaka azungumzie kauli ya Sitta kuwa muda wa Chadema kutawala nchi bado, kwa kuwa chama hicho hakina viongozi makini wa kufanya kazi za Serikali.

EBONY FM IRINGA YAFANYA MAHOJIANO NA MBUNGE WA IRINGA, MSIGWA



Akihojiwa nyumbani kwake na mtangazaji wa kituo cha Ebony FM, kupitia kipindi cha jambo beats na Bahati Alex. Mahojiano hayo yatakayo rushwa hivi karibuni katika kipindi cha jambo beats. Hivyo kaa tayari kujua nini Mbunge Msigwa akiongea katika mhojiano hayo.