To Chat with me click here

Tuesday, July 24, 2012

400 WAJIUNGA NA CHADEMA


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Morogoro kimeendelea kuzoa wanachama kutoka vyama mbalimbali ambapo juzi jumla ya wanachama wapya 400 walijiunga na chama hicho.Wanachama hao wapya walijiunga na Chadema katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya ‘Fire’ mjini hapa. Mwenyekiti wa chama hicho Manispaa ya Morogoro, Zuberi Kiloko, alisema kati ya wanachama hao 250 ni wapya huku 150 wakitoka Chama cha Wananchi (CUF) na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Awali, Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (Bawacha) Mkoa wa Morogoro, Levina Matambo na Katibu wa Bawacha, Mecy Naula, waliwashauri wanawake kubadilika na kuunga mkono juhudi za vyama vya siasa nchini kufanya mabadiliko ya kisiasa kwa kukiondoa chama kilichopo madarakani na kuingiza chama kipya.

Walisema utawala wa sasa unaongoza nchi kwa mazoea, jambo ambalo linaiingiza nchi kwenye matatizo mbalimbali likiwamo la ugumu wa maisha na huduma duni za kijamii.

No comments:

Post a Comment