To Chat with me click here

Saturday, July 7, 2012

JK AMPONGEZA BABA ASKOFU TARCISIUS NGALALEKUMTWA KWA KUTEULIWA KUWA RAIS WA TEC



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amempongeza Baba Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa (PICHANI) kwa kuteuliwa kwake kuwa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) akichukua nafasi ya Baba Askofu Yuda Tadei Rwaich aliyemaliza muda wake.

“Nimefarijika sana na uteuzi wako kushika wadhifa huo muhimu hasa kutokana na imani kubwa waliyonayo Maaskofu kuhusiana na uwezo wako katika kukiongoza chombo hicho muhimu”, amesema Rais Kikwete katika salamu zake.

“Ninatambua na kuthamini mchango mkubwa ambao, kwa muda mrefu sasa, Kanisa Katoliki limekuwa likuutoa kwa maendeleo ya nchi yetu, hasa katika Nyanja za huduma za jamii. 

Aidha uhusiano mzurpi kati ya serikali ninayoiongoza na Kanisa Katoliki unaendelea kunitia moyo, hivyo ninakuhakikishia kuwa Serikali ya Awamu ya nne itaendeleza nakuimarisha uhusiano huu kwa maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla”, amesema na kusisitiza Rais katika salamu zake za pongezi. 

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.

Dar-es-Salaam.

No comments:

Post a Comment