To Chat with me click here

Saturday, July 14, 2012

TANGAZO LA KAZI


 Kattikiro Internet Café & Stationary (Gongo la Mboto) ni moja ya ofisi bora zaidi inayotoa huduma ya Intaneti na Steshenari hapo Gongo la Mboto. Ofisi zetu ni ofisi zenye madhali nzuri kwa wafanyakazi. Ofisi hii ina kiyoyozi na imetengenezwa (designed) katika hali ya kisasa zaidi ili kuweza kukidhi mahitaji ya wateja wetu. 

Ofisi hii itafunguliwa tena hivi karibuni baada ya kuwa imefungwa kwa muda wa miezi michache iliyopita, hivyo tunahitaji wafanyakazi wawili wa kufanya kazi katika ofisi hii, wenye sifa na vigezo tunavyovihitaji. 

   Nafasi ya Kazi:                    Sekretari wa Ofisi
Atawajibika kwa:                  Mwajiri wake (Director)
Sehemu ya Kazi:                   Gongo la Mboto - Mzambarauni
Muda wa Kuanza Kazi:        Mara Moja

Kazi na Majukumu:
·        Kutoa huduma kwa wateja wetu wote kwa kuuza kulingana na maelekezo
·        Kutunza kumbukumbu za mauzo kwenye daftali husika
·        Kutoa ripoti juu ya matatizo yote ya hapo ofisini
·        Kuandaa listi ya vitu ambavyo vimeisha au kupungua pale ofisini
·        Kukamilisha majukumu mengine kama itakavyoelekezwa na mwajiri.
Vigezo na Taaluma:
· Awe mwenye umri usipungua miaka 18 na si zaidi ya miaka 35
· Awe na elimu ya Kidato cha nne na kuendelea
· Awe na uwezo wa kuongea Kiswahili na Kingereza vizuri
· Awe cheti, stashahada n.k toka  chuo kinachotambulika
·   Awe na uzoefu wa kufanya kazi na Steshenari kwa muda usiopungua mwaka mmoja.
· Ujuzi katika Adobe Photoshop, Publisher, Coral Draw na Multimedia na ujuzi wa Huduma za Intaneti ni siza za ziada ambazo zitatoa kipaumbele kwa aliye nazo. 

Malipo:
Katikiro Internet Café & stationary huwa tunawajali sana watu wetu, hivyo tumeandaa malipo mazuri kwa mtu yeyote atakaye kidhi vigezo vyetu. 

Namna ya Kutuma Maombi:
·        Tuma CV yako kwa: kattikirointernetcafe@gmail.com
·        Piga simu kwa namba hizi: +255 614 123160, +255 655 444666, +255 776 444666

 Mwisho wa kutuma maombi: ni mwezi mmoja tangu siku ya tangazo hili   (15/08/2012).

No comments:

Post a Comment