•  Wataka iundwe tume huru ya kuchunguza sakata zima 
CHAMA cha Madaktari Tanzania (MAT), kimepanga kufanya maandamano 
makubwa ya amani jijini Dar es Salaam ili kupinga dhuluma na uonevu 
dhidi ya taaluma muhimu ya udaktari na madaktari wenyewe.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu 
wa MAT, Dk. Rodrick Kabangila pichani, alisema maandamano hayo yatatanguliwa na 
mkutano mkubwa wa madaktari wote utakaofanyika leo kujadili mustkabali 
na mwenendo wa taaluma ya udaktari.
Kwa mujibu wa Dk. Kabangila, MAT inasikitishwa na dhuluma hiyo kwa 
kuzingatia uwiano duni wa madaktari hapa nchini ambapo daktari mmoja 
hutibu wagonjwa 30,000 kwa mwaka chini ya viwango vya kimataifa.
Alisema jumla ya madaktari 400 walio chini ya usimamizi wa madaktari 
bingwa, wamesitishiwa usajili wao na wengine kusimamishwa kazi bila 
kujali umuhimu wao kwa mustakabali wa taifa na wananchi wake.
“Tutafanya maandamano ya amani, madaktari wote na wadau wa sekta hii 
wenye mapenzi mema tunawaomba washiriki… madaktari tutavaa makoti yetu 
meupe na watakaoshiriki nasi wavae vitambaa vyeupe.
Maandamano yataanzia nje ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, tutaishia 
kwenye geti la Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, tukiwa na mabango ya 
kulaani kitendo cha kutekwa, kupigwa na kutelekezwa kwenye msitu wa 
Pande alichofanyiwa Dk. Steven Ulimboka,” alisema.
Dk. Kabangila alisema kuwa wataishinikiza serikali iunde tume huru kwa
 ajili ya kuchunguza suala la Dk. Ulimboka itakayofanya kazi haraka na 
wahusika wote wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.
Awali, katibu huyo alieleza kushangazwa kwake na wanaojiita viongozi 
wa dini ambao huwakatisha tamaa kwa kuwanena mabaya bila kujali 
mazingira magumu wanayofanyia kazi madaktari.
Mgogoro kati ya madaktari na serikali ulianza mwaka 2005 ambapo madai ya wataalam hao ni mazingira bora ya kazi, vitendeakazi bora, mashine za kisasa na nyongeza ya posho na mishahara.
Kushindwa kumalizika kwa mgogoro huo kulisababisha Jumuiya ya Madaktari nchini, kuitisha mgomo mwanzoni mwa mwaka huu ili kuishinikiza serikali kutimiza madai yao.
Mgogoro kati ya madaktari na serikali ulianza mwaka 2005 ambapo madai ya wataalam hao ni mazingira bora ya kazi, vitendeakazi bora, mashine za kisasa na nyongeza ya posho na mishahara.
Kushindwa kumalizika kwa mgogoro huo kulisababisha Jumuiya ya Madaktari nchini, kuitisha mgomo mwanzoni mwa mwaka huu ili kuishinikiza serikali kutimiza madai yao.

 
 
No comments:
Post a Comment