Kamanda wa polisi mkoa wa Singida,Linus Vicent Sinzumwa akizungumza na waandishi wa habari (hawapo kwenye picha) kutokana na vurungu zilizotokea kati ya wafuasi wa CHADEMA na CCM huko mkoani Singida.
Jeshi
 la polisi mkoa wa Singida linawashikilia wakazi 18 wa kata ya Ndago 
jimbo la Iramba magharibi kwa tuhuma ya kumuua mwenyekiti wa umoja wa 
vijana CCM (UVCCM) Yohana Mpinga (30) baada ya kumpiga kwa kutumia 
silaha za jadi.
Kamanda
 wa jeshi la polisi mkoa wa Singida Linus Vicent Sinzumwa amesema tukio 
hilo la kusikitisha limetokea Julai 14 katika kijiji cha Ndago.
Amesema
 siku ya tukio, Chama Cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) kilikuwa na 
kibali halali cha kufanya mkutano wa hadhara katika kijiji hicho cha 
Ndago na mgeni rasmi katika mkutano huo alikuwa mbunge wa jimbo la 
Ubongo jijini Dar-es-salaam Mhe. John J. Mnyika.
Mbali
 na Mnyika, viongozi wengine wa Chadema waliokuwapo ni Mjumbe wa Kamati 
Kuu ya Chadema, Dk Kitila Mkumbo na Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano 
wa chama hicho, Mwita Waitara.
Sinzumwa
 amesema mara baada ya CHADEMA kuanza mkutano huo, viongozi wake 
walianza kuporomosha mvua ya kashifa mbalimbali dhidi ya mbune wa jimbo 
hilo Mwingullu Nchemba, kitendo ambacho kiliudhi baadhi ya watu 
waliokuwa wamehudhuria mkutano huo.
Kamanda
 huyo amesema kuwa vurugu hizo zilihusisha kundi la wanachama wa CHADEMA
 na wa CCM na zilisambaa ambapo wanachama hao walianza kurusha mawe ovyo
 na askari wachache wa polisi waliokuwepo, walizidiwa nguvu na makundi 
hayo.
Amesema katika kundi hilo ambalo wamelikamata,watawahoji na wataobainika kuhusika watafikishwa mahakamani wakati wowote.
Akizungumza
 na waandishi wa habari, Mwita alidai mbali na mkutano huo kuwa na 
baraka za Polisi, lakini pia walikuwa na taarifa juu ya mpango wa 
kuvurugwa mkutano huo. Alidai
 waliwatahadharisha askari waliokuwapo kwenye eneo hilo kuwa kuna vijana
 ambao walikuwa wameandaliwa kufanya fujo ili kuhakikisha kuwa mkutano 
huo haufanyiki.
Kwa
 mujibu wa madai ya Mwita, taarifa hizo zilieleza kuwa kuna kikundi cha 
vijana kilichokuwa kimeandaliwa na kununuliwa pombe pamoja na kukodiwa 
gari ili kiharibu mkutano huo kwa kuhakikisha haufanyiki. Alidai
 pamoja kutoa taarifa hizo, hakuna hatua yoyote ya makusudi 
iliyochukuliwa na Polisi waliokuwapo karibu na eneo la mkutano, hali 
iliyosababisha fujo kutokea mara tatu kabla ya mkutano huo kuendelea na 
kukamilika salama na wao kuondoka katika eneo hilo.
“Lakini
 kutokana na vurugu zilizokuwa zikisababishwa na kikundi cha vijana 
ambao tayari walishatolewa taarifa yao kwenye mkutano huo mbele ya 
Polisi, askari waliokuwapo hawakuthubutu kuchukua hatua kwa vijana 
wale,” alidai Mwita. Alidai
 wakati wakiendelea na mkutano huo na baada ya kutoa taarifa kwa OCD na 
RPC, askari waliokuwa tayari kuzuia fujo walifika, lakini tayari fujo 
zilishatulia na mkutano uliendelea kama kawaida.
Kutokana
 na fujo hizo ambazo Mwita alidai zilitokea mara tatu, waliamua kufungua
 jalada Polisi lenye namba NDG/RB/190/2012 na katika jalada hilo 
walitaja majina ya watu waliokuwa wakifanya fujo mbele ya mkutano huo 
kwa lengo la kufanya mkutano huo usifanyike.
Aliwataja
 watu aliodai waliohusishwa na fujo hizo na walionaswa na kamera 
zilizokuwa zikitumiwa kuchukua kumbukumbu ya mkutano huo kuwa ni Daniel 
Sima, Tito Nitwa, Bakili Ayubu, Yohana Makala Mpande, Ernest Kadege, 
Abel John, Athumani Ntimbu, Martin Manase, James Ernest, Simon Makacha, 
Anthon John na Frank Yesaya.
“Kwa
 hakika askari wa Ndago waliokuwepo mkutanoni mbali ya kutochukua hatua 
yoyote, fujo za sisi kupondwa mawe zilizidi, askari wote walikimbia 
akabaki OCS pekee ambaye naye alionekana dhahiri kutochukua hatua 
stahili,” alidai Mwita.
Alisema
 mpaka wanaondoka katike eneo la mkutano hakukuwa na taarifa yoyote juu 
ya fujo ilizosababisha mtu kupoteza maisha na waliendelea na mkutano 
mwingine katika Kijiji cha Kinampanda na waliporudi hotelini walipofikia
 jioni mjini Singida walianza kusikia taarifa zinazoeleza kuwa kuna mtu 
au watu wamepoteza maisha katika mkutano wao wa  kwanza.
Mwita
 alidai Chadema inalaani taarifa zilizosambazwa kuwa chama hicho 
kinahusika katika kupoteza maisha ya mtu huyo kwani hakikujihusisha kwa 
aina yoyote katika kufanya fujo na muda wote kilikuwa kikiomba msaada 
kutoka kwa askari ili kutuliza fujo hizo.
Alisema
 kutokana na habari zinazosambazwa kwa kuihusisha Chadema, kuwa 
kinahusika katika kupoteza maisha ya mtu huyo, chama hicho kimebaini 
kuwepo mbinu chafu ya kuvihusisha vyombo vya Dola katika kuwatisha 
wananchi ili wasikiunge mkono katika kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya
 jamii.
Alisema
 tayari chama chake kimeshapokea taarifa kutoka Jeshi la Polisi ya 
kusitishwa kwa ziara yake ambayo kwa jana ingefanya mikutano miwili 
katika kijiji cha Shelui na Kiomboi na wanatii amri hiyo.


 
 
No comments:
Post a Comment