To Chat with me click here

Monday, November 19, 2012

KUUAWA NA KUPORWA KWA MAPADRE JE UJAMBAZI WA KAWAIDA AU NI MAHUSIANO NA VITA YA KIDINI DHIDI YA WAKRISTO NA WAISLAMU?

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge) William Lukuvi, amesema kuvamiwa, kupigwa risasi na kuporwa kwa mapadre wa Kanisa Katoliki Parokia za Isimani na Kihesa mkoani Iringa, ni ujambazi wa kawaida na hauhusiani na masuala ya udini.

Hadi kufikia jana mchana, tayari watu wanne akiwamo mwanamke mmoja, walikuwa wametiwa mbaroni, wakihusishwa na tukio hilo la uhalifu wa kutumia silaha.

Novemba 16, mwaka huu, zaidi ya watu sita waliokuwa na bunduki pamoja na silaha za jadi, walivamia Parokia ya Isimani na kuwapiga risasi, Paroko wa Kanisa hilo, Father Herman Myalla (36) na Angelo Burgio (66), raia wa Italia na baadaye kupora zaidi ya Shilingi milioni nne na Euro 100.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kuwajulia hali majeruhi hao waliolazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa, Lukuvi ambaye pia ni Mbunge wa Isimani, alisema waliohusika katika uhalifu huo ni majambazi na si vinginevyo.

”Kilichotokea ni ujambazi wa kawaida na hauhusiani na kitu kingine lakini pia tunaamini wote waliofanya uhalifu huo watafikishwa katika vyombo vya sheria. Nimewajulia hali na nimewahakikishia kwamba kilichotokea ni ujambazi tu kwa hiyo serikali iko pamoja nao,” alisema.

Katika tukio la kwanza lililotokea Novemba 15, mwaka huu majira ya usiku katika Manispaa ya Iringa, watu wasiofahamika walivamia na kupora vitu mbalimbali katika Parokia ya Kihesa na kumjeruhi vibaya mlinzi wa kanisa hilo, Bartholomeo Nzigilwa.

Hata hivyo, Kaimu Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Iringa, Dk. Gwanchelle Faustine, alisema jana kuwa hali za majeruhi watatu waliolazwa hapo zinaendelea vizuri.

No comments:

Post a Comment