To Chat with me click here

Saturday, November 17, 2012

DARAJA LA MJERUMANI LENYE MIAKA 100 IRINGA



Daraja hili ndilo linaunganisha vijiji vya Lundamatwe katika Manispaa ya Iringa na Wangama wilayani Iringa katika Mto Ruaha. Inaelezwa kwamba, daraja hili lenye miaka zaidi ya 100 lilijengwa enzi za Wajerumani miaka ya 1890 na bado linatumika hata sasa.



Hata hivyo, liko katika hali mbaya na halikidhi mahitaji ya wananchi. Kwa kifupi, ni hatari kwa usalama wa wananchi kwa vile limekwishazeeka kiasi kwamba ukipita linatingishika huku mbao zikionekana dhahiri kuchoka ingawa wananchi wanavuka kwa miguu, baiskeli na hata pikipiki.

Haijulikani kama mamlaka husika zinalitambua hili. Pengine zingeweza kuliboresha daraja hilo na kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kuwa na mawasiliano ya uhakika ya barabara tofauti na ilivyo sasa.

No comments:

Post a Comment