To Chat with me click here

Thursday, December 27, 2012

PADRI WA KIKATOLIKI APIGWA RISASI, AJERUHIWA WAKATI WA KRISMASI


Mtu mwenye silaha alimpiga risasi na kumjeruhi vibaya padri wa Kikatoliki Mjini Zanzibar siku ya Jumanne (tarehe 25 Disemba), liliripoti shirika la habari la AFP.

Padri Ambrose Mkenda, mkuu wa Kanisa la Kikatoliki la Tomondo, alipigwa risasi alipokuwa akirudi nyumbani kutoka kanisa lake kiasi cha saa 1:45 magharibi, alisema msemaji wa polisi wa Zanzibar Aziz Juma. Mkenda alipigwa risasi mkononi na kifuani kwa kutumia bastola.

Juma alisema haikufahamika mara moja ikiwa mashambulizi hayo yamechochewa na dini. "Uchunguzi unaendelea, lakini inawezakana pia kwamba washambuliaji walidhani padri huyo alikuwa na fedha," alisema.

Huku madaktari wakipigania kunusuru maisha yake, waumini wa Kikristo walikusanyika kwenye Hospitali ya Mnazi-Mmoja iliyo mji mkongwe wa Zanzibar. Wakristo ni asilimia 3 ya Wazanzibari milioni 1.2, wengi wao wakiwa ni Waislamu.

Hii ni mara ya pili kwa kiongozi wa kidini kushambuliwa ndani ya kipindi cha miezi miwili. Katibu Mkuu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhil Suleiman Soraga alijeruhiwa mnamo tarehe 6 Novemba pale alipomwagiwa maji yanaoaminika kuwa ni tindikali usoni na mwilini.

No comments:

Post a Comment