To Chat with me click here

Friday, January 4, 2013

ZANZIBAR YAPANGA MIRADI 62 YA MAENDELEO KUENZI SIKU YA UHURU


Zanzibar imepanga kuzindua miradi 62 ya maendeleo wakati wa wiki ya kuelekea siku ya uhuru tarehe 12 Januari, kwa kuanza na zoezi la kufanya usafi nchi nzima (tarehe 4 Januari). 

Siku ya Jumamosi, Rais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein atafungua jengo jipya la Taasisi ya Utawala wa Umma huko Tungu, na kituo kipya cha udhibiti wa serikali huko Mazini, yote yalijengwa kwa fedha kutoka serikali ya China. 

Makamu wa Rais wa Tanzania Mohamed Gharib Bilal atafungua hoteli ya kitalii ya nyota tano katika kijiji cha Nungwi siku ya Jumapili, na siku inayofuata ya Alhamisi Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete atafungua shule mpya inayoitwa Mlimani.

Viongozi mashuhuri wa serikali wa Zanzibar na Tanzania wataendelea kuongoza katika uzinduzi wa miradi kama hiyo kwa wiki nzima, ikiwa ni pamoja na shule za sekondari, maabara za uchunguzi na mabweni ya wanafunzi. 

Waziri wa Nchi anayeshughulikia Matukio ya Kitaifa Mohamed Aboud Mohamed alitetea sherehe hizo za muda mrefu, ambazo zinakadiriwa kugharimu shilingi milioni 600 (dola 380,000). "Tusifikirie kwamba fedha zinatumiwa kupita kiasi, zinatumiwa katika miradi ya maendeleo," alisema.

No comments:

Post a Comment