To Chat with me click here

Saturday, December 1, 2012

DAR ES SALAAM KUSIMAMISHA MABASI BINAFSI YANAYOTOA HUDUMA YA USAFIRI WA UMMA



Ofisa wa trafiki akiongoza msongamano wa dala dala kwenye barabara ya Uhuru katika eneo la Congo la Dar es Salaam.
Serikali ya Tanzania kuanzia Jumamosi (tarehe 1 Disemba) itaacha kutoa leseni kwa makampuni binafsi ambayo yanaendesha mabasi ya usafiri wa umma jijini Dar es Salaam, Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) ilitangaza.

Pia serikali haitahuisha leseni zilizopo kwa magari binafsi ya usafiri, hata hivyo, yataendelea kufanya kazi hadi vibali vyao vimalizike muda wa matumizi, kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa SUMATRA Ahmad Kilima.

Waendeshaji wa mabasi ya usafiri wa umma ambao wanataka kufanya kazi kama makandarasi wa serikali watapewa leseni za muda hadi mikataba itakapoanza kutumika mwezi Juni 2013.

Harakati hii ni sehemu ya mpango mkubwa wa kubadilisha mabasi madogo na mfumo wa mabasi ya umma yaendayo kasi unaosimamiwa na serikali. Serikali inategemea mpango wa usafiri mpya kuboresha usafiri wa umma, ukipunguza msongamano wa magari Dar es Salaam, ambapo SUMATRA inasema iliwagharimu Watanzania kiasi cha shilingi bilioni 4 (dola milioni 2.5 ) kila siku, kwa kuwa wasafiri wanapoteza muda mwingi kwenye msongomano wa magari.

Tangazo la Jumatano (tarehe 28 Novemba) lilikuja mwezi mmoja baada ya serikali kuzindua mfumo wa kwanza wa usafiri wa reli ya umma wa mji huo.

Mkurugenzi Mkuu wa Mabasi yaendayo Kasi Dar es Salaam Cosmas Tekule alisema usimamishaji wa kutoa leseni kwa takribani magari madogo 10,000 ya usafiri wa umma, yanayojulikana kama "dala dala", ulikuwa ni wa lazima kwa sababu hayana uhakika na yanasababisha msongamano na uchafuzi. 

"Tunaleta mabasi makubwa ambayo yatabeba hadi abiria 150," aliiambia Sabahi. "Kwa madaladala, yanayochukua abiria wapatao 30, unahitaji magari madogo matano ya abiria kuingia katikati ya mji kuchukua idadi hiyohiyo ya watu. Ni dhahiri, hii ni gharama kubwa." 

Alisema matumizi ya mafuta pia yatapungua kwa mabasi makubwa, kupunguza utoaji wa gesi ya kaboni, ambalo ni jambo zuri kwa mazingira. Mabasi mapya yanatarajiwa kuhudumia kiasi cha abiria 800,000 kila siku.

Zaidi ya hayo, serikali inajenga upya barabara kadhaa na kuweka barabara ya magari yaendayo kasi kwa mabasi mapya. 

Pontian Michael, mmiliki wa kampuni ya kuchomelea vyuma katikati ya jiji, aliiambia Sabahi kwamba uondoaji kwa awamu wa daladala utaboresha maeneo ya maegesho katika wilaya za biashara, ambayo alisema yamezuia wateja wanaotarajiwa.

MAANA YA HII KWA MADEREVA WA DALA DALA

Lakini madereva walisema mfumo mpya wa usafiri wa umma utapelekea kupoteza kazi kwa wengi miongoni mwao.

Mohamed Ibrahim, ambaye amekuwa akiendesha katika jiji kwa miaka 22, alisema wamiliki wengi wa mabasi ya usafiri wa umma ni wafanyabiashara wadogo ambao hawawezi kushindana dhidi ya wafanya biashara wakubwa kupata mkataba na serikali. "[Wamiliki wa makampuni makubwa] watawaajiri ndugu zao na karibia madereva wote wa dala dala wataachwa bila kazi," aliiambia Sabahi.

Michael Kakele, mmiliki wa dala dala anayesimamia Kampuni ya Kakele Transport, alisema kwamba waendeshaji binafsi wamekuwa katika mazungumzo na serikali kuhusu kipindi hiki cha mpito tangu mwaka 2010, na wanafurahia kufanya kazi katika muundo huu mpya. 

Lakini aliiambia Sabahi itakuwa vigumu kumudu gharama za ununuzi wa mabasi ambayo yatafikia viwango vipya, kwani yatagharimu hadi shilingi milioni 250 (dola 160,000), ambazo wamiliki hawawezi kukopa kirahisi katika benki. Serikali inaweza kuwasaidia wamiliki kupata mabasi na kupata sifa za mikataba kama itatoa dhamana ya mkopo kwa angalau wale wanaoendesha usafiri wa umma ambao walikuwa katika biashara kwa muda mrefu, alisema Kakele.

No comments:

Post a Comment