To Chat with me click here

Sunday, December 23, 2012

MBOWE: TUTAWASHUGHULIKIA WANATUVURUGA


MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe aweonya kuwa chama chake kitawachukulia watu wanatumiwa kutaka kukivuruga chama hicho huku akibainisha kwamba Chama chake hakina mpasuko wala mgogoro wa aina yoyote.

Akizungumza na wafuasi wa Chadema katika ofisi za makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam jana, Mbowe alisema chama hicho bado kipo imara na hakuna mpasuko kama ambavyo imekuwa ikidaiwa.

Mbowe alikuwa akizungumza na wafuasi hao ambao walifanya maadamano kutoka Mahakama ya Rufani hadi ofisi za chama hicho zilizopo Kinondoni, baada ya kada wa chama hicho, Godbless Lema kushinda rufaa yake iliyomrejeshea ubunge wa Arusha Mjini.

Mbowe alisema wapo baadhi ya watu wanaotumiwa kutaka kukivuruga Chadema kwa kueleza mambo yasiyo na ukweli lakini watambue kwamba Chadema hakiwezi kuyumbishwa na maneno ya watu na kwamba hakina mpasuko wala mgogoro wowote kama inavyo daiwa.

“Kuna watu wanasema kwamba Chadema kina mpasuko na mgogoro mkubwa lakini watu watambue kwamba Chadema kipo imara na kwamba hakiwezi kuyumbishwa na mtu yoyote yule mwenye nia mbaya ya kutaka kuvuruga Chama,” alisema Mboye na kuongeza:

“Chama chetu ni imara na kinachowajali wananchi na kwamba  sisi hatuwezi kusikiliza maneno ya watu wanaotaka kukivuruga chama kwa lengo la masilahi yao binafsi kwani lengo letu ni moja kutaka kuleta ukombozi wa kweli kwa  wananchi wa taifa hili.”

No comments:

Post a Comment