To Chat with me click here

Monday, December 31, 2012

WEDDING ANNIVERSARY


Mr. & Mrs. Kattikiro Jr
Kawaida ifikapo kila 31 December ya kila mwaka, kila mmoja duniani kote hukumbuka au kusherehekea kumaliza mwaka na kuanza au kuukaribisha mwaka mwingine unaoanza saa 6 kamili usiku wa siku hiyo. Kwetu sisi kama familia ya Mr. & Mrs. Kattikiro Junior tumekuwa tukikumbuka juu ya tukio la muhimu sana kwenye maisha yetu, kwani siku kama ya leo mwaka mmoja uliopita tuliweza kufunga ndoa takatifu katika kanisa kuu la Mt. joseph Jimbo Kuu la Dar-es-Salaam. 

Kwakweli tumepitia mengi katika mwaka huu mmoja wa maisha ya ndoa, pamekuwa na magumu mengi, lakini vilevile pamekuwa na neema nyingi mno. Mbali tu na Challenges nyingi za kimaisha lakini tumekutwa na misukosuko mingi katika maisha yetu ya kifamilia. Lakini kwa neema za Mungu tumeweza kuendelea kushikamana na kuweza kujikwamua kutoka katika matatizo na magumu hayo.

Kwa namna ya pekee kabisa tunapenda kuwashukuru wote ambao wamekuwa msaada mkubwa kwetu tangu tulipopata wazo la kufunga ndoa na kulikamilisha kulingana na taratibu za imani yetu hadi kufika leo hii ambapo tunaadhimisha mwaka mmoja wa ndoa. 

Tunawashukuru ndugu zetu wote, familia zetu, majirani na marafiki zetu wote kwa mshikamano, upendo, na misaada yao ya hali na mali wakati tulipo ihitaji. Tunaomba mzidi kutusaidia na kutuombea ili tuweze kudumu katika maisha ya ndoa. 

Lakini zaidi ya yote, tunatoa shukurani zetu za pekee kabisa kwa Mwenyezi Mungu, Baba yetu wa mbinguni, kwakuwa yeye ndiye amekuwa kiongozi wa familia yetu, amejalia wingi wa neema zako mno, zaidi tunamshukuru kwa kutupatia zawadi ya mtoto wa kike (Maureen Maxmillian Kattikiro). Kwakweli Jina la Mungu lihimidiwe.

Mwisho kabisa napenda kuwatakia furaha ya mwaka huu mpya na Baraka tele za Mungu Mwenyezi ziwe juu yenu nyote, ili sote kwa pamoja tuanze mwaka huu kwa amani na imani ya kufanikiwa zaidi. 

HAPPY NEW YEAR 2013 !!


MR. & MRS. KATTIKIRO JR.
31st DECEMBER 2012

No comments:

Post a Comment