To Chat with me click here

Thursday, December 27, 2012

MBOWE: HATUWEZI KUWA NA KATIBA MPYA


WAKATI Rais Jakaya Kikwete akiwaapisha wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Aprili 13 mwaka huu alionya kuwa mchakato wa kuandika Katiba Mpya usifanywe kwa kuegemea udini, ukabila, ubinafsi, siasa ama kulenga kuvunja Muungano.

Anasema maoni ya wananchi lazima yaheshimiwe hata kama hayataweza kuingizwa yote katika katiba hiyo, huku akiwataka wajumbe hao kuweka pembeni maslahi ya makundi wanayotoka kwa kuwa kazi wanayoifanya ni kwa maslahi ya taifa..

Tume hiyo ilianza kazi yake  ya miezi 18, Mei mosi mwaka huu, ambapo mpaka sasa imeshakusanya maoni katika mikoa takribani 15.

Mbali na kukusanya maoni ya wananchi na kutengeneza rasimu ya katiba, baadaye zitafuata  hatua mbili muhimu ambazo ni kuundwa kwa Bunge Maalumu la kuchambua rasimu hiyo, kisha wananchi kupiga kura ya maoni.

Tume hiyo ya Katiba jana ndio imemaliza kukusanya maoni ya Wananchi na kuanza kujipanga kwa taratibu nyingine za kumaliza kazi yake.

Pamoja na maelezo hayo ya Rais Kikwete watu wa kada mbalimbali likiwemo Jukwaa la Katiba Tanzania walipinga kwamba Katiba mpya haiwezi kupatikana Aprili 18, 2014 kama serikali inavyoeleza.

Wakipendekeza kwamba ili Katiba iweze kutumika ni lazima sheria nyingine zirekebishwe, zoezi ambalo huchukua miaka miwili.

Walisema kinachotakiwa kufanyika ni kurekebishwa kwa Ibara ya 98 ya Katiba ya sasa  katika vipengele vinavyohusiana na Tume ya Uchaguzi, ili uchaguzi wa mwaka 2015 uwe huru na wa haki, kuacha  mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya ukiendelea  kwa utaratibu mzuri.

Hoja hiyo ilinaonekana kuwagusa wengi na sasa,  Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe anasema jambo hilo linatakiwa kufanyiwa kazi haraka iwezekanavyo.

“Chadema tunaingiwa na hofu kwamba huenda Katiba mpya isiwe tayari kabla ya uchaguzi wa Serikali za mitaa mwaka 2014 na uchaguzi mkuu mwaka 2015” anasema Mbowe.

Anasema hakuna ulazima wa kupatikana kwa Katiba mpya katika kipindi hicho, badala yake mchakato huo uendelee lakini yafanyike marekebisho katika Sheria ya Uchaguzi ya mwaka 1985 ambayo ndani yake kuna Tume ya Uchaguzi (Nec) na daftari la kudumu la wapigakura.

“Kuna mambo yanatakiwa kufanyiwa kazi, kwanza ni kuwa na Tume huru ya Uchaguzi na mchakato wa kupata tume hii ufanyike bila kuathiri mchakato mzima wa kupata Katiba mpya.

No comments:

Post a Comment