To Chat with me click here

Sunday, May 19, 2013

IRINGA PACHAFUKA, MSIGWA AKAMATWA!



Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA) amekamatwa na polisi leo hii kwa tuhuma kuwa ndiye chanzo cha kuhamasisha wafanya biashara wadogo wadogo (wamachinga) kufanya vurugu huko Iringa.Askari polisi wa kutuliza ghasia (FFU) katika Manispaa ya mji wa Iringa pia imewakamata zaidi ya watu hamsini, akiwemoo aliyekuwa mgombea udiwani katika kata ya Mvinjini, Abuu Majeck.

Biashara zilisimama wakati wa sekeseke hilo, moshi ulitanda kutokana na matairi kuchomwa moto katika barabara za kuu ya Iringa-Dodoma na ile ya Mashine Tatu.

Leo hii pia, Mbunge huyo alikuwa katika eneo la chuo cha Tumaini kwenye harambee iliyokuwa imehudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.

No comments:

Post a Comment