To Chat with me click here

Tuesday, May 28, 2013

BREAKING NEWS: MSANII WA BONGO FLEVA AFARIKI DUNIA



Johannesburg, Afrika Kausini

                              Albert Mangwea enzi za Uhai wake R.I.P
TASNIA ya muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania (Bongo Fleva) imepata pigo baada ya msanii mahiri wa Hip Hop Albert Mangwea kufariki Dunia nchini Afrika Kusini.

Taarifa iliyonaswa na Vyanzo vyetu vya habari kutoka Afrika Kusini zinasema kwamba msanii huyo amefariki leo. "Alikuwa Ghetto Moja Na Msanii M To The P. ilipofika asubuhi ya leo hawakuweza kuamka mapema kama ilivyo kawaida yao na tulipokwenda kuwagongea tukakuta mlango wao uko wazi tuliingia ndani lakini hakuweza kuamka"alisema shuhuda wa tukio hilo.

Akizungumza na Vyanzo vyetu vya habari kwa nija ya simu akiwa nchini Afrika ya Kusini shuhuda wa tukio hilo alisema kwamba walipojaribu kuwatingisha hali haikuwa ya kawaida huku Mangwea akiwa ameshafariki Dunia na mwenzake M To The P akiwa hoi kiasi cha kupoteza fahamu.

Vyanzo vyetu vya habari ilimtafuta Hussein Oroginal aliyepo Pretoria ambaye alieleza kwamba hata yeye amepata taarifa za kifo cha Mangwea na tayari uchunguzi wa awali wa Madaktari umebaini kwamba wasanii hao walikuwa wamekunywa pombe nyingi kupita kiasi usiku wa kuamkia leo lakini haijajulikana kwamba pombe walizokunywa ni za aina gani.

"Nikweli Mangwea amefariki Dunia na tayari Madaktari wa Hospitali ya  St Hellena Joseph, ilipohifadhia mwili wa marehemu wanasema kwamba uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba. marehemu alikuwa amekunywa Pombe nyingi kupita kiasi, ingawa hawajaweza kusema kwamba pombe alizokunywa zilikuwa za aina gani," alisema mmoja wa ndugu wa karibu wa Marehemu Mangwea akiwa jijini Dar es Salaam, huku akiomba jina lake lisiandikwe mtandaoni kwakuwa yeye si msemaji wa familia.

No comments:

Post a Comment