To Chat with me click here

Friday, May 3, 2013

TEMBO WA TANZANIA KUTOWEKA NDANI YA MIAKA 7, MAAFISA WASEMA




Idadi ya tembo wa Tanzania aina ya jumbo inaweza kutokomezwa ndani ya miaka saba ikiwa ujangili utaendelea katika viwango vya sasa, mwenyekiti wa kamati ya bunge juu ya ardhi, mazingira na maliasili James Lembeli aliliambia Bunge la Taifa siku ya Jumanne (tarehe 30 Aprili). 

Kwa mujibu wa Taasisi ya utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI), Tanzania ilikuwa na tembo 109,000 mwaka 2009, lakini kuwa na kasoro ya tembo ya 70,000 mwaka 2012.

"Ikiwa mwenendo huu wa ujangili utaachiwa bila ya kushughulikiwa, ni wazi kuwa idadi ya tembo itapotea ndani ya miaka saba ijayo," Lembeli alisema kwa mujibu wa gazeti la The Guardian la Tanzania. "Hili ni janga la taifa. Serikali na mashirika yake inapaswa kuchukua hatua makini ili kushugulikia tatizo hili." 

Lembeli alitoa wito kwa serikali kuipitia Sheria ya Wanyamapori ya mwaka 2009, kutoa adhabu kali zaidi kwa majangili, kuajiri walinzi zaidi wa mbuga na kutoa vifaa na silaha za kisasa ili kupambana na ujangili.

Kwa dhamiri hiyo, aliomba bajeti ya kamati yake ya takriban shilingi bilioni 75.5 (dola milioni 46.5) kwa mwaka wa fedha 2013-2014. 

No comments:

Post a Comment