To Chat with me click here

Friday, January 4, 2013

TANZANIA YAAHIRISHA OMBI LA UUZAJI WA PEMBE ZA NDOVU



Tanzania imeahirisha ombi la kuuza zaidi ya tani 100 za pembe za ndovu ili kuendana na kanuni zilizowekwa na Mkataba wa Biashara ya Kimataifa ya Wanyama na Viumbe Vilivyo Hatarini (CITES).

Tanzania itaongeza udhibiti dhidi ya uwindaji haramu na kuimarisha vikwazo vya magendo ya pembe za ndovu kabla ya kutuma tena ombi lake. Serikali pia itafanya sensa ya idadi ya tembo kujua kiwango cha wanyama hao nchini humo, kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Utalii na Maliasili.

Tanzania imeomba kuuza pembe za ndovu zilizomo kwenye ghala yake, zilizopatikana kutokana na tembo waliokufa vifo vya kawaida au waliouliwa kwa sababu ya kuhatarisha maisha ya wanadamu, ili kugharamia vyema programu zake za ulinzi wa rasilimali.

CITES ilikataa ombi kama hilo la serikali ya Tanzania mwaka 2010, ikihoji kwamba kuzipeleka pembe hizo sokoni kungeliongeza, na sio kupunguza, visa vya uwindaji haramu.

No comments:

Post a Comment