To Chat with me click here

Wednesday, January 9, 2013

POLISI WA TANZANIA WAKAMATA SILAHA HARAMU 439


Msemaji Msaidizi wa Jeshi la Polisi Nchini ASP Advera Senso

Polisi nchini Tanzania walikamata silaha haramu 439 kutoka kwa raia katika operesheni ya mwezi mmoja ya kukusanya silaha zisizo vibali, alitangaza msemaji wa polisi Advera Senso hapo Jumatatu. 

Operesheni hiyo ya polisi, iliyomalizika tarehe 5 Januari, iliwapa Watanzania fursa ya kusalimisha silaha zao haramu bila ya kushitakiwa, liliripoti gazeti la The Guardian la Tanzania. Miongoni mwa silaha zilizosilimishwa ni bunduki ndogo, bunduki kubwa, bastola, risasi na maroketi.

Sasa polisi wataanzisha msako wa nchi nzima na kuwakamata watu wanaoendelea kukaa na silaha bila ya ruhusa maalum.

Polisi iliwatolea wito raia kutoa taarifa juu ya yeyote mwenye silaha kinyume na sheria. Mtanzania yeyote atakayetoa taarifa inayopelekea kukamatwa kwa mtu atapewa zawadi ya kiasi cha shilingi 100,000 (dola 63), alisema Senso.

Kati ya visa 876 za wizi wa silaha mwaka jana nchini Tanzania, 62 vilifanywa kwa silaha haramu, kwa mujibu wa gazeti la The Guardian.

No comments:

Post a Comment