To Chat with me click here

Wednesday, January 2, 2013

WASANII WA FILAMU WAENDELEA KUPOTEZA WENZAO: SAJUKI NAYE AFARIKI

Aliyekuwa Msanii maarufu katika tasnia ya filamu nchini Juma Kilowoko (SAJUKI) enzi za uhai wake kabla ya kukumbwa na maradhi.
SAJUKI enzi za uhai wake baada ya kuwa amekwishaanza kusumbuliwa na maradhi
Msanii Sajuki akiwa hospitali akiendelea kupata matibabu kutokana na tatizo la kupungukiwa damu.

Aliyekuwa Msanii maarufu katika Tasnia ya Filamu nchini Juma Kilowoko almaarufu kama  ’SAJUKI’ aliyekuwa akisumbuliwa na maradhi ya muda mrefu amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Kwa mujibu wa taarifa toka kwa Katibu wa chama cha waongoza filamu wilaya ya Ilala Bw. Rajabu Amiri amesema kuwa marehemu alikuwa akisumbuliwa na tatizo la upungufu wa damu hivi karibuni.

Maxmillian Kattikiro Blog: Inaungana na Familia ya Marehemu pamoja na Watanzania wote katika Kuombeleza Kifo cha Mpendwa wetu Marehemu SAJUKI… Inalilahi Wainalilahi Rajiun.

TAARIFA ZAIDI ZITAKUJIA HAPO BAADAE. ENDELEA KUPERUZI Maxmillian Kattikiro Blog.

No comments:

Post a Comment