To Chat with me click here

Thursday, January 31, 2013

MAKINDA AMPONGEZA LEMA


SPIKA wa Bunge Anna Makinda, amempongeza Mbunge wa Arusha Mjini, Goodbless Lema (CHADEMA) kwa kurejea bungeni.

Spika alitoa pongezi hizo jana ndani ya Ukumbi wa Bunge baada ya kumuona mbunge huyo akiingia ukumbini na kuketi kwenye kiti chake.
“Naona Mheshimiwa Lema anaingia. Nachukua nafasi kukupongeza kwa kurudi bungeni. Karibu sana,” alisema spika huku wabunge wengine wakishangilia kwa kupiga makofi.

Lema, mmoja wa wabunge machachari wa CHADEMA, alikuwa nje ya Bunge kwa takribani miezi kumi baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kumvua ubunge.

Kesi dhidi yake ilifunguliwa na wanachama sita wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambao pamoja na mambo mengine walidai Lema alimkashifu mgombea wao, DkBatilda Burian.

Hata hivyo, Lema alikata rufaa na kurejeshewa ubunge wake Desemba mwaka jana.

Tayari Lema ameahidi kufufua hoja zote alizoziacha bungeni, ikiwemo hoja kwamba Waziri Mkuu alilidanganya Bunge.

No comments:

Post a Comment