To Chat with me click here

Tuesday, February 12, 2013

CHAMA CHA UPINZANI TANZANIA CHATISHIA KUANDAMANA DHIDI YA WIZARA YA MAJI




Chama cha upinzani cha Tanzania CHADEMA kimetishia kuandamana mbele ya Wizara ya Maji kuchochea serikali kuchukua hatua kuhusiana na upungufu mkubwa wa maji jijini Dar es Salaam, gazeti la Daily News la Tanzania liliripoti.

Mbunge wa Ubungo John Mnyika alitangaza kusudio la chama kupinga wakati wa matembezi kutoka eneo la Veterinari hadi viwanja vya Temeke Mwisho jijini Dar es Salaam. Waandamanaji wamempa Waziri wa Maji Jumanne Maghembe wiki mbili kufafanua mbele ya umma wizara inafanya nini kushughulikia matatizo ya maji jijini.

Mwaka jana, utafiti ulionyesha kwamba karibia asilimia 77 ya wakaazi wa Dar es Salaam hawapati maji ya kutosha. Maghembe aliliambia bunge kwamba serikali imepanga kuwa na zaidi ya mara mbili ya usambazaji wa maji jijini Dar es Salaam ifikapo mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment