To Chat with me click here

Friday, June 22, 2012

MKONO AIBUA UFISADI KIWIRA

Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, ameibua ufisadi unaodaiwa kufanywa katika mgodi wa Kiwira na kulitaka Bunge kuunda kamati maalumu ya uchunguzi.

Mkono alidai kuwa sehemu moja ya mgodi huo yenye utajiri mkubwa imeuzwa kwa bei ya kutupwa kwa kampuni moja ya Australia.

Alisema uuzaji huo ni kinyume cha makubaliano yaliyofikiwa na Bunge  mwaka 2007 ambapo liliagiza kuwa mgodi wa Kiwira uliokuwa umeuzwa kwa Kampuni ya Tan Power urudishwe serikalini baada ya kuwa umeuzwa kwa dola laki saba tu.

Hata hivyo, Mkono alisema kuwa katika hali ya kushangaza Kampuni ya Tan Power ambayo ilikuwa imeingia ubia na serikali iliuzwa kwa Waustralia  kiasi cha mabilioni ya dola. “Mheshimiwa Spika, Kiwira kulikoni? Lini Bunge litaunda kamati ya kwenda kuangalia Kiwira?” alihoji na kusema kuwa pamoja na yote hayo, sasa serikali imetenga sh bilioni 40 kwa ajili ya mradi wa Kiwira na kuhoji nani aliteketeza fedha za awali zilizotolewa kwa ajili hiyo.

No comments:

Post a Comment