Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, ameibua ufisadi unaodaiwa 
kufanywa katika mgodi wa Kiwira na kulitaka Bunge kuunda kamati maalumu 
ya uchunguzi.
Mkono alidai kuwa sehemu moja ya mgodi huo yenye utajiri mkubwa imeuzwa kwa bei ya kutupwa kwa kampuni moja ya Australia.
Alisema uuzaji huo ni kinyume cha makubaliano yaliyofikiwa na Bunge  
mwaka 2007 ambapo liliagiza kuwa mgodi wa Kiwira uliokuwa umeuzwa kwa 
Kampuni ya Tan Power urudishwe serikalini baada ya kuwa umeuzwa kwa dola
 laki saba tu.
Hata hivyo, Mkono alisema kuwa katika hali ya kushangaza  Kampuni ya 
Tan Power ambayo ilikuwa imeingia ubia na serikali iliuzwa kwa 
Waustralia  kiasi cha mabilioni ya dola. “Mheshimiwa Spika, Kiwira kulikoni? Lini Bunge litaunda kamati ya 
kwenda kuangalia Kiwira?” alihoji na kusema kuwa pamoja na yote hayo, 
sasa serikali imetenga sh bilioni 40 kwa ajili ya mradi wa Kiwira na 
kuhoji nani aliteketeza fedha za awali zilizotolewa kwa ajili hiyo.

 
 
No comments:
Post a Comment