Bajeti ya Mwaka huu 2012/2013 ni Bajeti ya Madeni
Serikali inapendekeza Bajeti ya TZS 15 trilioni(USD 8.75 Billion)
katika mwaka 2012/13. Uchambuzi wa vitabu vya Bajeti unaonesha kwamba
mafungu ya juu 5 kwenye Bajeti ni Kama ifuatavyo;
1 Huduma kwa Deni la Taifa Tshs 2.7 trilioni(USD 1.69 Billion)
2 Wizara ya Ujenzi. Tshs 1 trilioni (USD 625 Million)
3 Wizara ya Ulinzi Tshs 920 bilioni (USD 575 Million)
4 Wizara ya Elimu Tshs 721 bilioni (USD 451 Million)
5 Wizara ya Nishati na Madini Tshs 641 bilioni (USD 400 Million)
TOTAL TZS 5.982 Trilioni(USD 3.74 Billlion)
Chanzo: Vitabu vya Bajeti kwa Wabunge
Jumla ya mafungu haya ni sawa na asilimia 40% ya Bajeti. Kwa hiyo
asilimia 40% ya Bajeti yote imepangwa kwa mafungu 5 tu. Fungu lenye
kiwango kikubwa zaidi ya Bajeti kuliko vyote ni fungu 22 ambalo ni
malipo kwa Deni la Taifa. Pia sehemu kubwa ya fedha zilizotengwa kwa
Ujenzi na Nishati ni madeni kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi ya
miaka ya nyuma.
Hii yaweza kuwa Bajeti ya kulipa madeni zaidi kuliko Bajeti ya
kuchochea maendeleo. Bajeti hii pia yaweza pia kuwa ni Bajeti ya kukopa
maana jumla ya TZS 5.1 trilioni(USD 3.19 Billion)
zitachukuliwa kama mikopo kwa Serikali. Mikopo ya kibiashara ambayo ni
mikopo ghali sana itachukuliwa kwa wingi zaidi kuliko mwaka wa fedha
uliopita.
Wabunge wanapaswa kufanya uchambuzi zaidi wa Bajeti ya mwaka huu
inayopendekezwa na Serikali. Kuna haja kubwa sana ya kuharakisha
kuanzishwa kwa Ofisi ya Bajeti katika Bunge na Kamati ya Bunge ya Bajeti
ili kuweza kufuatilia kwa karibu, kuchunguza na kutoa taarifa kwa
wabunge ili kuwezesha kuboresha Bajeti.
Misamaha yote ya Kodi na Madeni yote ambayo Serikali inaingia inabidi
sasa ithibitishwe na Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi ili kuongeza
udhibiti na usimamizi wa Misamaha ya Kodi na pia Deni la Taifa.
No comments:
Post a Comment