 To Chat with me click here
To Chat with me click here
          
        
          
        
CHADEMA UKONGA TISHIO KWA CCM - JIMBONI
Chama
 cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jimbo la Ukonga kinayo heshima 
kubwa sana kuwataarifu ndugu Wananchi wa Jimbo la Ukonga kwa ushirikiano
 mkubwa waliouonesha wakati wa Mikutano ya hadhara ambapo chama-Jimbo 
kilipokea takribani wanchama 50 toka CCM na vyama vingine.
 Chama – 
Jimbo la Ukonga kimekuwa kikiendea kufanya mikutano ya hadhara kwenye 
kata mbalimbali na kuwapokea wanaCCM wengi na kufanya ongezeke la 
wanachama wapya kuwa kubwa mno hivyo kukipelekea Chama Jimbo kukosa 
uwezo wa kuendelea kuendesha mikutano ya hadhara pia kukabiliana na 
ongezeko hilo, ingawa kuna taratibu na harakati ambazo tunaendelea nazo 
ili kuhakikisha tunawakaribisha vyema wanachama hao wapya na kuongeza 
kasi ya mapambo ili kuendelea kupata wanachama wengi zaidi.
 
 
Mpaka sasa tumeshafanya mikutano na kupokea waliokuwa wanachama wa CCM 
katika kata za Kitunda, Ukonga, Chanika na Majohe. Vilevile tunategemea 
tarehe 03/06/2012 kufanya mkutano mwingine mkubwa wa kuwapokea wanachama
 wapya wanaotokea CCM na vyama vingine katika kata ya Pugu, na mpaka 
sasa kuna matawi matatu ya CCM kata ya Ukonga na Kivule ambayo 
yamekwisha omba kutaka mikutano ya hadhara ili wasalimimshe kadi na 
uanachama wa CCM kwa viongozi wa Chadema Jimbo.
 
 Ni imani yetu 
sisi wanaCHADEMA-Ukonga na viongozi wake kuwa, sasa kazi imeanza na 
hakuna kulala mpaka kieleweke maana kwa utaratibu huu unaoendelea kwenye
 chama uongozi wa Taifa, tunaamini kuwa kata na majimbo mengine mengi 
yatafuata mwenendo huu kwani wamekuwa wakionesha ari hiyo ya kukihama 
chama tawala.
 
 27/05/2012 CHADEMA tumepokea wanachama zaidi ya 
hamsini (50) na uongozi mzima wa matawi wa kata ya Majohe, ambao 
wamejiunga na chama chetu. Zipo taarifa zaidi kuwa kuna matawi mengine 
mawili ya chama cha mapinduzi (CCM) yamepania kujiunga na CHADEMA hivi 
karibuni tena kwenye moja ya mikutano ya hadhara ambayo tunategemea 
kuifanya.
 
 Hivyo tunawaomba wananchi wote wenye mapenzi mema na 
chama (CHADEMA) na wenye uzalendo wa kutosha kutuunga mkono katika 
jitihada zetu za ukombozi wa nchi toka kwenye makucha ya wajanja 
wachache ili kuleta maendeleo ya kweli na maisha bora kwa umma wa 
watanzania, ili tuweze kufikia malengo hayo kwa urahisi zaidi. 
Tunakaribisha michango yenu ya hali na mali hata mawezo yenu ya 
kuboresha na kukiimalisha chama zaidi katika hili.
 
 Wenu katika ujenzi wa Taifa/Chama
 
 Kny. Katibu Jimbo la Ukonga.
 Maxmillian Kattikiro.
 
 
 
          
      
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment