To Chat with me click here

Friday, June 1, 2012

CHADEMA UKONGA TISHIO KWA CCM - JIMBONI

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) jimbo la Ukonga kinayo heshima kubwa sana kuwataarifu ndugu Wananchi wa Jimbo la Ukonga kwa ushirikiano mkubwa waliouonesha wakati wa Mikutano ya hadhara ambapo chama-Jimbo kilipokea takribani wanchama 50 toka CCM na vyama vingine.
Chama – Jimbo la Ukonga kimekuwa kikiendea kufanya mikutano ya hadhara kwenye kata mbalimbali na kuwapokea wanaCCM wengi na kufanya ongezeke la wanachama wapya kuwa kubwa mno hivyo kukipelekea Chama Jimbo kukosa uwezo wa kuendelea kuendesha mikutano ya hadhara pia kukabiliana na ongezeko hilo, ingawa kuna taratibu na harakati ambazo tunaendelea nazo ili kuhakikisha tunawakaribisha vyema wanachama hao wapya na kuongeza kasi ya mapambo ili kuendelea kupata wanachama wengi zaidi.

Mpaka sasa tumeshafanya mikutano na kupokea waliokuwa wanachama wa CCM katika kata za Kitunda, Ukonga, Chanika na Majohe. Vilevile tunategemea tarehe 03/06/2012 kufanya mkutano mwingine mkubwa wa kuwapokea wanachama wapya wanaotokea CCM na vyama vingine katika kata ya Pugu, na mpaka sasa kuna matawi matatu ya CCM kata ya Ukonga na Kivule ambayo yamekwisha omba kutaka mikutano ya hadhara ili wasalimimshe kadi na uanachama wa CCM kwa viongozi wa Chadema Jimbo.

Ni imani yetu sisi wanaCHADEMA-Ukonga na viongozi wake kuwa, sasa kazi imeanza na hakuna kulala mpaka kieleweke maana kwa utaratibu huu unaoendelea kwenye chama uongozi wa Taifa, tunaamini kuwa kata na majimbo mengine mengi yatafuata mwenendo huu kwani wamekuwa wakionesha ari hiyo ya kukihama chama tawala.

27/05/2012 CHADEMA tumepokea wanachama zaidi ya hamsini (50) na uongozi mzima wa matawi wa kata ya Majohe, ambao wamejiunga na chama chetu. Zipo taarifa zaidi kuwa kuna matawi mengine mawili ya chama cha mapinduzi (CCM) yamepania kujiunga na CHADEMA hivi karibuni tena kwenye moja ya mikutano ya hadhara ambayo tunategemea kuifanya.

Hivyo tunawaomba wananchi wote wenye mapenzi mema na chama (CHADEMA) na wenye uzalendo wa kutosha kutuunga mkono katika jitihada zetu za ukombozi wa nchi toka kwenye makucha ya wajanja wachache ili kuleta maendeleo ya kweli na maisha bora kwa umma wa watanzania, ili tuweze kufikia malengo hayo kwa urahisi zaidi. Tunakaribisha michango yenu ya hali na mali hata mawezo yenu ya kuboresha na kukiimalisha chama zaidi katika hili.

Wenu katika ujenzi wa Taifa/Chama

Kny. Katibu Jimbo la Ukonga.
Maxmillian Kattikiro.

No comments:

Post a Comment