To Chat with me click here

Thursday, June 14, 2012

MWONGOZO WA BAJETI - KATTIKIRO (Sehemu - 2)

Mchakato wa Bajeti katika Serikali za Mitaa
 
Tanzania Bar inazo wilaya 133, manispaa, majiji na miji. Hii huunda Mamlaka za Serikali za Mitaa (Local Government Authorities), na kila mamlaka ina halmashauri yake iliyochaguliwa. LGA husaidia kutoa huduma za jamii kama vile elimu, huduma za afya, upatikanaji wa maji vijijini, kilimo na barabara. Wajumbe   wa halmashauri yaani madiwani huchaguliwa na wananchi na hukuwakilisha wewe pamoja na mahitaji yako. Ni wajibu wao kutetea mahitaji yako pamoja na kupigania haki zako kwenye vikao vya halmashauri. Wanawajibika kukupatia taarifa zote muhimu.

Nani anawajibika katika mchakato wa Bajeti ya serikali za mitaa?
Wadau mbalimbali wanahusika katika mchakato wa bajeti ya serikali za mitaa kama inavyooneshwa hapa chini.
·         Mkutano Mkuu wa Kijiji
·         Halmashauri ya Kijiji
·         Baraza la Kata
·         Wakurugenzi wa Halmashauri / Viongozi wa Halmashauri
·         Sekretarieti ya Mkoa
·         Serikali Kuu
·         Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI

Wizara katika ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI huandaa sera na miongozo inayosimamia uendeshaji wa serikali za mitaa.

Serikali kuu kupitia wizara husika (Kama vile Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii) huandaa sera zinazosimamia sekta zinazohusika.

Sekretarieti ya mkoa chini ya usimamizi wa Afisa Tawala wa mkoa (Regional Secretariate) huunganisha serikali kuu na mamlaka za serikali za mitaa. Sekretariati ya Mkoa hutoa taarifa za miongozo ya namna ya kupanga, kuandaa bajeti pamoja na utekelezaji wake.

Katika ngazi ya serikali za mtaa, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na uongozi wa Halmashauri husimamia utekelezaji wa bajeti kama ilivyopangwa. Halmashauri (inayojumuisha madiwani na wabunge) huijadili bajeti pamoja na kuikubali au kuipitisha.

Kamati ya maendeleo ya Kata (Ward Development Committee) Ni kiunganishi kati ya vijiji, vitongoji na halmashauri ya wilaya. Wajumbe wa kamati hii hujumuisha diwani wa kata, afisa mtendaji wa kata na wenyeviti wa vijiji. Kamati ya maendeleo ya Kata (WDC) hukutana kila baada ya miezi mitatu. Pia inaweza kukutana mara nyingi zaidi kama itaonekana kuna umuhimu wa kukutana.

Halmashauri ya Kijiji (Village Council) inahusisha Mwenyekiti wa kijiji au kitongoji pamoja na viongozi wengine wanaochaguliwa na mkutano mkuu wa Kijiji. Mkutano mkuu owa Kijiji hujumuisha wanawake na wanaume wenye miaka 18 na kuendelea. Kila mwanakijiji aliye mtu mzima humiliki Mali za Kijiji kama vile ardhi, misitu na njia za usafiri wa majini. Kwa mujibu wa sheria, halmashauri ya kijiji inapaswa kukutana walau mara nne kila mwaka. Kwa upande wa majiji, manispaa na miji kuna baraza la manispaa na mtaa.

Fedha zinatoka wapi?
Fedha katika bajeti za mitaa zinapatikana kutokana na vyanzo viwili: Mapato ya nje na mapato ya ndani.

Mapato ya nje:
Hizi ni fedha kutoka serikali kuu ambazo ni karibu asilimia 90 ya bajeti nzima ya serikali za mitaa. Vyanzo vya mapato hayo ni vya aina tofauti tofauti.

Ruzuku
Kila halmashauri inapewa ruzuku na serikali kuu kwa ajili ya matumizi ya kawaida (ambayo hujumuisha malipo ya mishahara pamoja na gharama zingine za uendeshaji) katika kila sektabmuhimu ya kijamii (afya, elimu, maji katika vijiji, kilimo na barabara) pamoja na ruzuku ya uendeshaji. Ruzuku inapaswa kutumika kama ilivyoelekezwa na serikali kuu na si vinginevyo. Kwa wastani asilimia 60 ya bajeti ya serikali za mitaa inategemea ruzuku.

Mfuko wa fedha kwa ajili ya sekta maalumu
Hizi ni fedha za ziada za matumizi ya kawaida zinazotolewa kulenga sekta Fulani muhimu zilizopo chin ya wizara husika.  Kwa mfano fedha kwa ajili ya Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) na fedha kwa ajili ya Mfuko wa pamoja wa huduma za afya (Healthy Sector Basket Fund). Fedha hizi hutolewa ili kusaidia maendeleo ya kilimo pamoja na huduma za afya. TACAIDS hutoa fedha katika halmashauri zote kwa ajili ya kugharamia miradi ya VVU/UKIMWI.

Fedha kupitia mkakati  wa uchumi na kuondoa umaskini Tanzania
(MKUKUTA)- fedha hizi hutolewa kwa ajili ya shughuli za maendeleo zikilenga kupunguza umasikini. Fedha hizi kwa kawaida zinatumika kuboresha miundombinu pamoja na vipaumbele vingine vilivyowekwa na halmashauri. Piafedha hizi hutumika kujenga uwezo wa serikali  za mitaa pamoja na shughuli za maendeleo  kama vile ujenzi  wa vyumba vipya  vya madarasa, huduma  za afya, miradi ya maji vijijini, ujenzi wa barabara mpya n.k.

Vipaumbele vinapangwa na wewe mwananchi wakati mchakato wa kuainisha fursa na vikwazo vya maendeleo (Opportunity and Obstacles to Development). Kwa wastani, fedha hizi huchukua asilimia 17 ya bajeti nzima ya mwaka ya halmashauri.

Misaada maalumu ya maendeleo-misaada hii kwa kawaida hulenga mikoa, sekta au maeneo maalumu na ina malengo maalumu. Kwa mfanomradi wa uwezeshaji katika kilimo (PADEP), mradi wa uwekezaji katika kilimo ngazi ya wilaya (GASIP), mradi wa Hifadhi ya Mazingira na maendeleo ya mji (UDEM), mradi wa ushirikishwaji katika maendeleo ya misitu (Participatory Forest Management), mradi wa uhifadhi wa ardhi endelevu (Sustainable Wetland Management), Ruzuku ya usafirishaji katika wilaya na vijiji (LGTP/VTTP), Ruzuku ya maendeleo ya Halmashauri na shirika la kimataifa la kuhudumia watoto UNICEE. Fedha hizi huchangia wastani wa asilimia 5 ya bajeti ya mwaka ya serikali za mitaa.

Fedha za ziada
Fedha zingine pia katika halmashauri utolewa na washirika wa maendeleo, miradi na mipango maalum ya serikali au michango ya watu binafsi. Halmashauri ya Kijiji (VC) inapaswa ifahamu kuhusu fedha hizi.

Mapato ya ndani: mapato haya hupatikana ndani ya wilaya na kwa kawaida huwa ni asilimia 10 ya bajeti nzima.
Kodi za serikali za mitaa: Serikali itaa vile vile hupata fedha kutokana na kodi mbalimbali zinazotozwa. Taarifa hiyo hapo chini inaorodhesha vyanzo hivyo vya mapato. Kwa wastani, kodi hizi huchangia asilimia 8 ya bajeti zao za mwaka.

Mapato ya ndani ya serikali za mitaa

Kodi za vitu
·         Kiwango

Kodi kwenye vitu vya huduma
·         Ushuru wa mazao (Kiwango cha juu ni 5% ya bei ya shambani)
·         Ushuru wa mazao ya misitu

Kodi kutokana na za utaalamu
·         Ushuru  wa nyumba za kulala wageni

Leseni za biashara na za utaalamu
·          Ushuru wa uvuvi wa kibiashara
·         Ushuru wa leseni kwa huduma binafsi ya afya
·         Ushuru wa leseni za teksi
·         Ushuru wa leseni ya usafirishaji mizigo
·         Ushuru wa leseni nyingine za biashara

Magari
·          Ushuru wa leseni za magari
·         Ushuru wa leseni ya vyombo vya uvuvi

Kodi zingine kwa ajili ya matumizi ya vitu, ruhusa kutumia vitu.
·         Ushuru wa leseni za bidhaa za misitu
·         Ushuru wa uchimbaji wa vifaa vya ujenzi
·         Ushuru wa leseni za uwindaji
·         Ushuru wa leseni ya kumiliki silaha
·         Ushuru wa matangazo

Kodi za mapato
·         Ushuru wa huduma

Mapato yatokanayo na umiliki wa  vitu pamoja na shughuli za ujasiliamali
·         Gawio
·         Mapato mengine ya ndani na miliki
·         Riba
·         Ukodishaji ardhi

Vyanzo vingine vya mapato
·         Ada za shughuli za kiutawala
·         Faini, adhabu na mali zinazotelekezwa
  
MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA HAZIRUHUSIWI KUTOZA KODI YA AINA YOYOTE AMBAYO HAIPO KWENYE ORODHA HII 

Michango ya jamii
Hii ni ya jamii nzima. Kutegemeana na aina ya miundombinu, mfano darasa, michango hii inaweza kuwa na tofauti kati ya asilimia 2.5 hadi 30 ya gharama zote ingawa mara nyingi ni asilimia tano. Michango hii inatakiwa itumike kwa ajili ya kuendeleza miundombinu ambayo
imepewa kipaumbele na jamii kupitia zoezi la utambuzi wa fursa na vikwazo vya maendeleo 
(O & OD).

Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF)
Huu ni mpango wa ubia kati ya serikali na Benki ya Dunia unaolenga kutoa fehda kwa ajili ya miradi ya miundombinu pamoja na kutoa ajira za muda mfupi. Ubia huu umelenga kuwashirikisha wananchi katika Nyanja za barabara, kupitia mipango ya maendeleo ya jamii ikilenga kuboresha huduma za jamii kama vile maji au mpango wa jamii unaolenga kutoa huduma kwa makundi yanayoishi mazingira hatarishi, kwa mfano kutoa mafunzo kwa watu wenye ulemavu.

Mfumo huu ni mgumu, kwa mfano shule inaweza kupokea fedha kutoka kwenye vyanzo vingi ambavyo ni tofauti kama inavyoonesha hapo chini. 
  • Ruzuku 
  • GBS
  • Ruzuku ya Ziada 
  • Fedha za Maendeleo 
  • MMEM
  • Michango ya Jamii 
  • Local Government Capital Development Grant (LGCDG)  
NB: Tafadhali usikose mwendelezo wa Mwongozo huu Kesho. 

No comments:

Post a Comment